UKAWA WATISHIA KUANDAMANA

Umoja wa viongozi wa katiba ya wananchi (UKAWA) umetishia kuanzisha maandamano makubwa hadi ikulu, endapo Rais nchini na Mwenyekiti wa Tume ya kurekebisha daftari la wapiga kura, hawatafanya marekebisho kabla ya chaguzi zijazo.

Hayo yamesemwa na makatibu wakuu wa vyama vya upinzani nchini, kikiwemo chama cha CHADEMA, CUF na NCCR, ambapo wamesema watanzania milioni tano na laki nane hawana vitambulisho vya kupigia kura.

Vyama hivyo vimewataka viongozi husika, kufanya jitihada za kurekebisha daftari hilo, ili chaguzi zijazo ziwe za huru na haki