PALESTINA KULITAMBUA TAIFA LA ISRAEL

Rais wa Palestina, Mahmuoud Abbas amesema serikali ya pamoja itakayowajumuisha kundi la Hamas, italitambua taifa la Israel na wajibu wa kitaifa pamoja na kutangaza kusimamisha machafuko.

Bwana Abbas amelimbia baraza kuu la chama cha kisiasa cha PLO, kwamba bado angelipenda kuendelea na mazungumzo ya amani na Israel.

Israil imesimamisha mazungumzo hayo baada ya kutangazwa kwa serikali ya pamoja ambayo itaongozwa na bwana Abbas na Hamas wanaotawala himaya ya ukanda wa Gaza.

Rais wa Palestina ametetea makubaliano hayo ya serikali ya pamoja na kusema hawezi kuwabana na kuwakana raia wake walioko Gaza na wala kukataa kuendelea na mazungumzo ya amani na Israil.