KIVUMBI CHA AFCON 2015 KUANZA KUTIMKA

Droo ya Kufuzu kwa kombe la mataifa bingwa Barani Afrika mwakani{ Afcon} imefanyika huko cairo Misri huku timu zote za kanda ya Afrika Mashariki zikiratibiwa kucheza katika mechi za mchujo kabla ya kushiriki mechi za kufuzu.

Kenya itachuana dhidi ya Visiwa vya Comoro ,Tanzania ipambane na Zimbabwe, Uganda imeratibiwa kutoana kijasho dhidi ya Madagascar nayo Rwanda ikivaana na Libya.

Raundi ya Kwanza

*.Liberia v Lesotho

*.Kenya v Comoros Islands

*.Madagascar v Uganda

*.Mauritania v Equatorial Guinea

*.Namibia v Congo

*.Libya v Rwanda

*.Burundi v Botswana

*.Central African Republic v Guinea Bissau

*.Swaziland v Sierra Leone

*.Gambia v Seychelles

*.Sao Tome e Principe v Benin

*.Malawi v Chad

*.Tanzania v Zimbabwe

*.Mozambique v South Sudan

Burundi kwa upande wake itachuana dhidi ya Botswana, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ikiratibiwa kuvaana na Namibia.

Baada ya kushiriki mkondo wa kwanza wa maondoano mataifa hayo tena yatalazimika kuchuana miongoni mwao ilikufuzu kwa awamu ya pili.

Mshindi wa mkondo huo wa pili ndio watakao jumuishwa katika makundi saba yaliyotajwa jana.

Raundi ya Pili

Liberia or Lesotho v Kenya or Comoros Islands

Madagascar ,Uganda v Mauritania ,Equatorial Guinea

Namibia , Congo v Libya , Rwanda

Burundi , Botswana v CAR , Guinea Bissau

Swaziland or Sierra Leone v Gambia , Seychelles

Sao Tome e Principe or Benin v Malawi , Chad

Tanzania , Zimbabwe v Msumbiji , Sudan kusini

Mechi za raundi ya kwanza zitang'oa nanga tarehe 6-18 Mei.

Mechi za marudio zitasakatwa wikiendi ya tarehe 30-31 Mei hadi Juni Mosi.

Katika mechi zitakazoibua hisia ni pamoja na mabingwa watetezi Nigeria ambao wameratibiwa kuvaana na Afrika Kusini.

Mahasimu wa jadi kaskazini mwa Afrika Tunisia na Misri wameratibiwa kukwaruzana nayo Ghana,ikitoana kijasho na Togo.

Aidha Ivory Coast itafungua kampeini yake ya kufuzu kwa dimba hilo lenye hadhi baranidhidi ya mahasimu wao wakuu Cameroon.

Droo ya Makundi:

Kundi A :
Nigeria,
Sudan,
South Africa
{Namibia vs Congo Brazzaville/Libya vs Rwanda}

Kundi B:
Mali,
Ethiopia,
Algeria
{ Sao Tome e Principe vs Benin/Malawi vs Chad}

Kundi C:
Burkina Faso,
Gabon,
Angola
{ Liberia vs Lesotho/Kenya vs Comoros Islands}

Kundi D:
Ivory Coast,
Democratic Republic of Congo,
Cameroon
{ Swaziland vs Sierra Leone/Gambia vs. Seychelles}

Kundi E:
Ghana,
Guinea,
Togo
{Madagascar vs Uganda/Mauritania vs Equatorial Guinea}

Group F:
Zambia,
Niger,
Cape Verde Islands
{ Tanzania vs Zimbabwe/Mozambique vs South Sudan}

Kundi G:
Tunisia,
Senegal,
Egypt
{ Burundi vs Botswana/ Central African Republic vs Guinea Bissau}

Mechi za makundi zitaandaliwa kati ya tarehe 5-6 Septemba na tarehe 10 Septemba.

Mkondo wa pili utaandaliwa kati ya tarehe 14-15 November na 19 November.

Washindi wawili katika kila kundi watajiunga na wenyeji Morocco mwakani kwenye kipute cha kuwania taji la taifa bingwa barani Afrika 2015.