SHERIA YA KUOA WAKE WENGI YAPITA KENYA

Sheria inayoruhusu wanaumekuoa wake zaidi ya mmoja, imepitishwa nchini Kenya.

Rais Uhuru Kenyatta ametia saini sheria hio licha ya malalamiko kutoka kwa vikundi vya wanawake nchini humo.


Taarifa kutoka katika ofisi ya Rais ilisema kuwa mswada huo ambao unaojumuisha vipengele kadhaa kuhusu ndoa , imekuwa sheria sasa.

Mswada huo ulioleta mageuzi katika sheria ya sasa , ilipitishwa na bunge mwezi jana kuidhinisha rasmi utamaduni wa ndoa ya zaidi ya mwanamke mmoja.


Taarifa ya Rais ilisema kuwa"ndoa ni muungano wa watu wawili mwanamke na mwanamume , ikiwa mume atataka kuoa mke mmoja au wawili, mwenyewe anapaswa kuamua. ''Mswaa wa awali, ulimpa mwanamke haki ya kwenda mahakamani kupinga mume wake kuoa mke wa pili, lakini wabunge wanaume waliungana katika kuunga mkono mswada huo.

Wakati mswada huo ulipopitishwa mwezi jana , wabunge wanawake waliondoka bungeni kwa Hasira baada ya mjadala mkali.

Viongozi wa baadhi ya makanisa pia wamepinga vikali mswada huo


Shirikisho la kitaifa la mawakili wanawake pia limesema kuwa litapinga sheria hiyo mahakamani.


Katika sehemu nyingi barani Afrika, kuoa zaidi ya mwanamke mmoja ni jambo la kawaida katika tamaduni nyingi sawa na hali ilivyo nchini Kenya na hata pia miongoni mwa waumini wa dini ya kiisilamu.

Wengi wanasema kuwa sheria hiyo inapiga tu muhuri wa utamaduni uliopo.