MAKOMANDO KUWASAKA WAPIGANAJI UKRAINE

Vikosi vya jeshi nchini Ukrain vimekuwa vikielekea mji wa Slavyask ambayo ni ngome ya makundi ya wapiganaji wanaounga mkono Urusi.

Wizara ya masuala ya ndani nchini Ukraine inasema kuwa imeharibu vizuizi vitatu vilivyowekwa na makundi haramu yaliyojihami kwenye mji wa mashariki wa Slavyansk.


Wizara hiyo inasema kuwa watu watano waliotajwa kuwa magaidi wameuawa.

Waziri wa masuala ya ndani nchini Ukrain Arsen Avakov amesema kuwa vikosi vya serikali vimefanikiwa kuwaondoa wanamgambo wanaoiunga mkono Urusi kutoka kwa majengo ya serikali katika mji wa Kusini Mashariki wa Mariupol.

Duru zinasema kuwa aneo la kati mwa Sloviansk ni tulivu.


Wapiganaji wanaotaka kujitenga na Ukraine wakati wakiunga mkono Urusi, wameendelea kuteka majengo ya serikali mjini humo.

Awali maafisa nchini Urusi walikuwa wameonya Ukrain kutokan na kuwachukulia hatua makundi yaliyojitenga.


Naye rais wa Marekani Barack Obama alinukuliwa awali akisema kuwa Urusi haikutii makubaliono ya Geneva yaliyokuwa na lengo la kuzima mzozo nchini Ukrain.