MADUKA YATEKETEA NA MOTO DODOMA

Maduka matatu makubwa yameteketea kwa moto na mengine yameathirika katikati ya mji wa Dodoma baada ya jengo linalodaiwa kumilikiwa na mamlaka ya uendelezaji makao mkuu-CDA kuwaka moto.


Katika maduka hayo yaliyokuwa mkabala na makao makuu ya cmm na kukuta moto mkubwa ukiendelea kuteketeza, huku vikosi vya zimamoto na jeshi la polisi vikifanya jitihada za kukabiliana na moto huo husivamie maduka mengine huku baadhi ya wamiliki wa maduka wakiondoa bidhaa zilizomo ndani ya baadhi ya maduka kwa hofu ya moto huo kuingia katika maduka yao.

Akizungumza mkuu wa wilaya ya Dodoma bwana Lify Gembe amesema chanzo cha moto huo bado hakijajulikana, na inaseemekana moto huo umeanza katika duka moja linalouza vipodozi.

Kwa upande wake mkuu wa kikosi cha zimamoto mkoa wa Dodoma Sajenti Meja Amri Issa amesema umbali wa eneo ya kuchukua maji na uchakavu wa vifaa umesababisha zoezi la kukabiliana na moto huo kuchukua muda mrefu na kuwataka wamiliki wa maduka kuhakikisha wanaweka vifaa vya kuzimia moto.

Wakizungumza baadhi ya wamiliki wamelalamikia kikosi cha zimamoto kukosa vifaa huku mipira ya maji ikionekana kutoboka hali inayosababisha maji kuvuja barabarani, huku wengine wakidai askari wanashindwa kupanda juu ya magari zimamoto ili kunusuru baadhi ya mali za watu zisiteketee.