WAFANYA BIASHARA WAVAMIA GHALA LA HALMASHAURI YA JIJI

Vurugu kubwa za wafanyabiashara wadogo jijini Arusha maarufu kama wamachinga wamevamia ghala la manispaa ya jiji kwa lengo la kutaka warudidshiwe mali zao hatua iliyozua tafrani kubwa iliyosababisha naibu meya kupigana na baaadhi ya mgambo wa jiji waliokuwa wanajaribu kuwadhibiti wananchi hao.

Katika tafrani hiyo mgambo wa jiji aliyetajwa kwa jina la Marry Msuya amejeruhiwa na kulazwa hosipitali akidai kuwa amepigwa na naibu meya Mh Prosper Msofe huku naibu meya aliyekuwa anawatetea wananchi hao naye akidai kuwa amepigwa na mgambo huyo .

Baadhi ya wananchi wamelaalamika kuwa wamekuwa wakipigwa na kuporwa mali zao hata wakiwa wanatembea barabarani bila kuvunja sheria zilizowekwa.

Mkurugenzi wa jiji Bw Juma Iddy amesema suala la wananchi kupigwa halikubaliki lakini suala la zoezi la kusafisha jiji ni endelevu na amesisitiza kila mmoja kuheshimu sheria.