BUS LA HOOD LATEKETEA KWA MOTO

Abiria zaidi ya 55 wamenusurika kufa baada ya basi la Hood kuungua moto likiwa safarini kutoka mkoani Mbeya kwenda Arusha.


Zaidi ya abiria 55 waliokuwa ndani ya basi la kampuni ya Hood, wakisafiri kutoka Mbeya kwenda Arusha walinusurika kufa baada ya basi hilo kushika moto na kuteketea kabisa katika kijiji cha Kilolele, Chalinze mkoani Pwani.

Kufuatia ajali hiyo ya moto ya basi la Hood, mpaka sasa chanzo cha moto huo hakijaelezwa.


Julai 2011, Kampuni hiyo ya mabasi ya Hood iliungua moto karibu na hifadhi ya Mikumi mkoani Morogoro ambapo watu watano walikufa kwenye basi hilo lililokuwa na namba za usajili T 762 AVL lililokuwa likitoka Mbeya kwenda Arusha.


Katika ajali hiyo abiria 40 walijeruhiwa vibaya sehemu mbalimbali za miili yao na kukimbizwa katika Hospitali ya Mkoa ya Morogoro kwa matibabu.