WAFANYAKAZI STRABAG WAGOMA WAKIDAI POSHO

Mradi wa mabasi yaendayo haraka huenda usikamilike kwa wakati kutokana na migomo ya mara kwa mara ndani ya kampuni hiyo ambapo zaidi ya wafanyakazi elfu moja wamegoma kushinikiza uongozi wa kampuni hiyo kuwalipa posho zao za takribani miezi nane ambazo zimedaiwa kulipwa kwa ubaguzi kwa baadhi ya wafanyakazi kutoka nje ya nchi.


ITV imefika makao makuu ya kamuni hiyo Strabag jijini Dar es Salaamu na kuwakuta wafanyakazi wakiwa wamezagaa huku ofisi za uongozi wa kampuli hiyo zikiwa zinalindwa na askari wenye silaha za moto ambapo baadhi ya wafanyakazi hao wamesema wameamua kugoma ili kushinikiza kampuni hiyo kuwalipa posho zao za zaidi ya miezi nane ambazo wamekuwa wakipigwa danadana bila kujua hatma yao.


Aidha wafanyakazi hao wameendelea kulaani kitendo cha uongozi wa kampuni hiyo kuendelea kulipa posho hizo kwa wafanyakazi wengine waliotoka nchi jirani bila kutambua ya kuwa posho hizo zipo kisheria na imesainiwa kwenye mikataba yao ambpo wanadai kila mfanyakazi zaidi ya laki tano huku wakiiomba serikali kuingilia kati ili waweze kupata haki yao.


Jitihada za ITV za kutafuta uongozi wa kampuni hiyo ili kufafanua juu ya madai ya wafanyakzi hao ziligonga mwamba baada ya baadhi ya viongozi kugoma kuongea na wengine kujifungia ndani.

Chanzo:ITV