WAKIMBIZI WAUAWA KATIKA KAMBI S.KUSINI

Afisa mkuu wa Umoja wa mataifa nchini Sudan kusini Tobby lanzer ameiambia BBC kuwa makumi ya wakimbizi wa ndani ya nchi hiyo iliyosakamawa na vita vya wenyewe kwa wenyewe wameuawa ndani ya kambi ya Umoja wamataifa iliyoko katika mji mkuu wa jimbo la Jonglei BOR.

Afisa anayesimamia shughuli za utoaji misaada ya umoja wa mataifa nchini sudan toby Lanzer amesema kuwa kundi la vijana wanaokisiwa kuwa zaidi ya mia tatu hivi walikuja katika kambi hiyo wakidai kuwa walitaka kuwasilisha malalamiko, kwa wasimamizi wa kambi hiyo. Toby alisema '' Ilikuwa mwendo wa saa nne hivi katikati ya mji mkuu wa jimbo la jonglei BOR ambapo vijana takriban 350 hivi walikusanyika na kuanza kuandamana hadi kwenye ualakambi yetu mara wakavunja lango kuu na kuingia ndani ya kambi.

Maafisa wetu walifyatua risasi ilikuwatawanya lakini wao pia wakaanza kufyatua risasi kiholela na katika tafrani iliyotokea wavamizi hao waliwashambulia wakimbizi waliokuwa wametorokea katika kambi yetu wakati wamapigano yaliyozuka desemba."

Mjini Bor Afisa huyo alilaanitukio hilo akisema ni jambo la kuhuzuzisha kwa watu waliokimbilia usalama ndani ya kambi ya umoja wa mataifa wakivamiwa humo humo na kuwa Umoja wa mataifa sasa utachukua tahadhari zaidi ilikuzuia matukio kama hayo katika siku za usoni.

''Tumeimarisha hali ya usalama katika kambi zetu ilikuwazuia wale wote wenye niya ya kutudhuru sisi na kuanzia sasa tunatoa tahadhari kwa makundi yote kuwa tutatumia nguvu kadri na uwezo wetu ilikuzuia matukio kama hayana kulinda maisha ya wale wote ambao wametorokea hapa ilikuokoa maisha yao''.

Maafisa 2 wa kulinda usalama wa umoja wa mataifa walijeruhiwa vibaya katika shambulizi hilo.

Kambi ya BOR imehifadhi zaidi ya wakimbizi 5000 tangu mwezi Desemba majeshi ya serikali ya rais Salva Kiir yalipoanza makabiliano na makundi ya wapiganaji wanaomuunga mkono aliyekuwa makamu wa rais wa nchi hiyo Riek Machar.