AFISA MKUU WA POLISI AUWAWA MISRI

Maafisa wa usalama nchini Misri wanasema afisa wa ngazi ya juu wa polisi nchini Misri ameuawa katika shambulio la bomu katika mji mkuu Cairo.

Polisi huyo Brigedia Generali Ahmed Zaki aliuawa katika kitongoji cha Magharibi mwa mji huo baada ya bomu lililokuwa limetegwa chini ya gari lake kulipuka.

Shambulio hilo ni la hivi karibuni katika mfululizo wa mashambulizi dhidi ya vikosi vya usalama tangu kung'olewa madarakani kwa aliyekuwa Rais Mohamed Morsi Mwezi Julai mwaka jana

Mjini Alexandria,afisaa mwingine mmoja aliuawa wakati wa shambulizi dhidi yakile maafisa wanasema ni maficho ya wanamgambo.

Wapiganaji wa kiisilamu wameongeza kasi ya mashambulizi dhidi ya maafisa wa usalama na kuwaua mamia tangu jehi kumwondoa mammalakani Morsi.

Mnamo siku ya Jumapili, mtu aliyekuwa amejihami kwa bunduki alimpiga risasi na kumuua afisaa mmoja wa polisi aliyekuwa anashika doria.

Shambulizi hilo lilitokea siku moja baada ya polisi mwingine kuuawa mjini Cairona kundi la wapiganaji wajulikanao kama Ajnad.

Kundi hilo linasema linashambulia polisi kwa sababu ya msako unaofanywa dhidi ya kundi la Muslim Brotherhood. Zaidi yawatu 1,300 wameuawa na wengine 16,000 kuzuiliwa.

Ghasia hizi huenda zikatishia usalama wakati wa uchaguzi mkuu utakaofanyika mwezi Mei, ambapo aliyekuwa mkuu wa majeshi Abdul Fattah al-Sisi anatarajiwa kushinda.