MAMA NA MWANAE WAFARIKI KWA KUPIGWA NA RADI

Mpanda Katavi

Wanawake wawili mama na Mtoto wake wakazi wa Kijiji cha Mnyagala Tarafa ya Kabungu Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi wamefariki Dunia baada ya kupigwa na Radi na Kufa hapo hapo wakati wakiwa njiani wakiwa wanatokea kwa jirani yaoKwa mujibu wa Kamanda wa Jeshi la Polisi wa Mkoa wa Katavi Kamishina mwandamizi Msaidizi Dhahiri Kidavashari alisema tukio hilo lilitokea hapo A prili 22 mwaka huu majira ya saa kumi na mbili jioni kijijini hapo

Kamanda Kidavashari aliwataja waliokufa kwa kupigwa na Radi ni Migu Samwel 46 na mwanae wakike aitwaye Nsungulwa Kasanzu 15 wote wawili wakiwa wakazi wa kijiji hicho cha Mnyagala


Alisema kabla ya vifo hivyo vya mama na mwanae marehemu hao walikuwa wamekwenda kwa jirani yao kwa lengo la kumsalia na wakati wako huko waliona wingudogo la mvua likiwa limetanda hewani


Alieleza kutokana na kuwepo kwa wingu hilo dogo la mvua marehemu hao walimuaga jirani yao kuwa wanawahi kurudi nyumbani kwao kabla mvua ya haija anza kunyesha kwani waliondoka nyumbani huku baba mwenye nyumba akiwa hayupo alikuwa amekwenda kwenye shughuli zake za ufundi wa baiskel kijijini hapo katika eneo linaloitwa Center


Alifafanua wakati wakiwa wanaelekea i walipofika jirani na nyumba yao umbali wa mita 15 ndipo walipopigwa na radi na kufa hapo hapo ambapo mama alipigwa na radi sehemu ya kifuani na mwanae alipigwa na radi sehemu ya kichwani


Alisema baada ya kuwa wamepigwa na Radi na kufafa hapo hapo miili ya marehemu hao iliokotwa na majirani walikuwa wakipita kwenye eneo hilo baada ya mvua ndogo ilinyesha kuwa imekatika


Kidavashari alieleza majirani hao baada ya hapo walitowataarifa kwenye uongozi wa Serikali ya Kijiji ambao nao walifika kwenye eneo hilo nakisha walitowa taarifa za vifo vya marehamu hao kwa jeshi la polisi Wilaya ya Mpanda


Alisema miili ya marehemu hao ilitarajiwa kuzikwa jana kijijni hapo mara baada ya taratibu za kidaktari zitakapokuwa zimekamilika na jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi limetowa wito kwa wakazi wa Mkoa huo huacha kutembea barabarabi wakati wa mvua na waepuke kupita karibu na miti