MCHINA AJINYONGA KWA KUBORONGA KAZI

Raia mmoja wa China ambaye ni mhandisi katika Kampuni ya Ujenzi ya China Railway Bureua 15 Group inayojenga Daraja la Mto Kilombero, Qin Bao Feng amekufa kwa kujinyonga kwa kile kinachodaiwa ni baada ya kuboronga katika kazi.


Ilielezwa kuwa Feng aliamua kujinyonga baada ya nguzo za daraja alilokuwa akilisimamia katika ujenzi huo, kusombwa na maji, jambo ambalo aliona kuwa limemvurugia kazi yake.


Baadhi ya watu waliokuwa jirani na kambi hiyo, walisema baada ya kuharibika kwa kazi hiyo, wahandisiwenzake kutoka China, walianza kumtenga hali iliyomfanya ajione kuwa mpweke na hatimaye kuchukua uamuzi huo.


Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Leonard Paulo alisema tukio hilo lilitokea Jumamosi iliyopita ndani ya kambi ya kampuni hiyo.


Alisema mwili wa marehumu ulikutwa ukining'inia kwenye dari ndani ya chumba alichokuwa analala na kwamba polisi wanaendelea na uchunguzi wa kina kuhusu tukio hilo.


Kamanda Paulo alisema baada ya kuchunguza mwili wa marehemu walikuta karatasi iliyokuwa imeandikwa ujumbe kwa lugha ya Kichina.


Alisema kwa kuwa hakuna mkalimani aliyekuwa jirani na eneola tukio, polisi wanaendelea kumtafuta mtu wa kuutafsiri.


Alisema kwa sasa mwili wa marehemu huyo umehifadhiwa katika Hospitali ya St Francis iliyopoKilakala, Morogoro.