MAJAMBAZI WAVAMIA KAMBI YA WACHINA NA KUJERUHI

Watu wanane wanaosadikiwa kuwa majambazi wakiwa na siraha za jadi mapanga na marungu wamevamia kambi ya Kampuni ya wachina wanaotengeneza Barabara kwa kiwango cha rami ya kutoka Mpanda hadi Sitalike Wilayani Mlele Mkoa wa Katavi na kumjeruhi mlinzi wa Kampuni hiyo Kwa mujibu wa Kamanda wa Jeshi la Polisi wa Mkoa wa Katavi Kamishina mwandamizi msaidizi Dhahiri Kidavashari alisema tukio hilo lilitokea hapo Aprili 22 mwaka huu majira ya saa tano na dakika thelathini na tano usiku katika kambi ya kampuni hiyo iliyoko katika Eneo la kata ya Magamba Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi.

Alisema siku hiyo ya tukio watu hao wanane wanaosadikiwa kuwa ni majambazi walifika kwenye kambi hiyo na kisha walimvamia mlinzi wa kampuni hiyo Joseph Sarangi na kumshambulia kwa kutumia silaha za jadi mapanga na marungu na kumjeruhi kwenye paji la uso na kichwani kufanikiwa kuiba betrii la gari aina ya Nissan lenye Namba 120 na kisha kutokomea kusikojulikana.


Alieleza kuwa jeshi la Polisi lilipata taarifa ya tukio hilo baada ya muda mfupi baada ya kuwa limetokea kwenye eneo hilo na walianza wawafatilia watu hao waliohusika na tukio hilo la ujambazi wa kutumia silaha hizo za jadi.

Kamanda Kidavashari alisema katika msako huo wa Jeshi la polisi siku hiyo hiyo walifanikiwa kumtia mbaroni mtuhumiwa mmoja aitwaye Juma Athumani 23 Mkazi wa Mtaa wa Tambukaleli Mjini hapa.

Alisema baada ya kumkamata mtuhumiwa huyo mmoja jeshi hilo bado linaendelea kuwatafuta watuhumiwa wengine saba ambao walishiriki kwenye tukio hilo la ujambazi wa kutumia silaha za jadi.


Aidha alieleza kuwa mtuhumiwa Juma Athumani anatarajiwa kufikishwa Mahakamani mara baada yaupelelezi wa tikio hili utakapo kuwa umekamilika ili sheria iweze kuchukua mkondo wake wa sheria