ZAIDI YA WATU 10 WAFARIKI NA WENGINE 44 WAJERUHIWA KATIKA AJARI YA GARI

Zaidi ya watu 10 wamefariki dunia papo hapo na wengine 44 kujeruhiwa baada ya basi la Luwuye express walilokuwa wamepanda likitoka Tarime kwenda Mwanza kuacha njia na kuparamia nyumba na kupinduka katika kijiji cha Itwimila wilaya ya Busega mkoani Simiyu.


ITV ilifika katika eneo la tukio mara tu baada ya ajali hiyo kutokea na kukuta umati mkubwa wa watu ambao wengine ni wakazi wa kijiji hicho cha Itwimila a, kitongoji cha Inchira, kata ya Kirureli wilaya ya Busega mkoani Simiyu na wengine ni abiria waliokuwa wakisafiri na basi hilo la Luhuye express yenye namba za usajili t.410 awq inayodaiwa kuwa ilikuwa ikitoka tarime kuelekea mwanza.


Licha ya ITV kushuhudia baadhi ya miili ya watu waliopoteza maisha katika ajali hiyo huku idadi ya watu waliojeruhiwa ikionekana kubwa zaidi, baadhi ya watu wamedai basi hilo ilikuwa ikiendeshwa kwa mwendo kasi sana lakini ilipofika katika eneo hilo, ghafla tairi ya mbele ya gari hilo ilipasuka na kusababisha basi hilo kuacha njia na kupinduka mara kadhaa na kuvamia nyumba ya mkazi wa eneo hilo ambalo limejengwa pembezoni mwa barabara kuu ya kuelekea Mwanza.


Kutokana na maumivu makali, baadhi ya abiria ambao ni majeruhi walionekana wakiomba msaada kwa watu ili kukimbizwa katika hospitali mbalimbali za jirani jambo ambalo itv kwa kushirikiana na mashuhuda walifanikisha kulifanya huku gari ya polisi moja nalo likiwa limefanikiwa kufika katika eneo la tukio kutoa msaada ambapo baadhi ya majeruhi waliingizwa katika gari kwa ajili ya kukimbizwa hospitalini.


Baadhi ya watu wameonekana kupoteza maisha huku wengine wakilaliwa na tairi za gari na wengine wameonekana kuvunjika sehemu mbalimbali ya miili baada ya kuangukia nje kupitia madirisha ya busi hilo.

ITV ilizungumza na kamanda wa polisi mkoa wa Simiyu SACP Charles mkumbo kwa njia simu na kithibitisha kutokea kwa ajali hiyo huku akidai kuwa idadi ya walipoteza maisha kwa upande wa wanawake ni wanne, wanaume walipoteza maisha ni sita na mtoto ni mmoja huku idadi ya majeruhi akidai kuwa ni 44 ambapo wanawake ni 19 na wanaume ni 25 na kwamba majeruhi wamekimbizwa katika hospitali ya rufaa ya bugando jijini mwanza na wengine katika hospirtali ya wilaya ya magu huku chanzo cha ajli hiyo akidai haijajulikana na kwamba dereva wa basi hilo hajaonekana hivyo hawana uhakika iwapo amefariki au amekimbia kwani kuna mtu alionekana akikimbia wakati wa ajali ila haijajulikana iwapo ni dereva wa basi hilo au lah.

Chanzo: ITV