BUNGE LA KATIBA MPAKA AGOSTI 5

Bunge maalum la katiba limeahirishwa hadi agasti tano mwaka huu huku wabunge wa wakitahadharishwa kuacha kumshambulia aliyekuwa mwenyekiti wa iliyokuwa tume ya mabadiliko ya katiba jaji mstaafu Joseph Warioba au mjumbe yeyote binafsi wa iliyokuwa tume ya mabadiliko ya katiba.


Akitoa maoni kabla ya kuahirishwa kwa bunge hilo,mwanasiasa mkonge ambae pia ni mbunge wa bunge hilo, Mhe Kingunge Ngombare Mwiru, amewaomba wajumbe hao kuacha kushambulia mtu na wasitumie msimamo wa CCM kufanya hivyo kwani wanakitukanisha Chama cha Mapinduzi.

Aidha kuhusu kero zilizomo katika katiba ya sasa, Mhe Kingunge amesema kero kubwa kwa wananchi ni umasikini hivyo ametaadharisha katiba yeyote itakayo andikwa bila ya kukabili tatizo la umasikini itakuwa si katiba bora.


Kwa upande wake makamu wa pili wa rais wa Zanzibar Mhe, balozi eif Ali Idd amesema serikali inatumia zaidi ya milioni 188 kila siku kwa kazi ya katiba ambapo sasa rais kwa ridhaa yake ameongeza siku 60 hivyo ni vyema wapunguze mijadala isiyoyalazima na kuzionea huruma fedha za walipa kodi.

Waziri mkuu mhe. Mizengo pinda amesema anashangzwa na baadhi ya watu wanao dai tanganyika wakati ilidumu kwa kipindi mwaka mmoja na nusu na kuwataka wabunge wasiwabeze wahasisi wa muungano wa tanzania,huku spika wa baraza la wawakilishi Mhe. Pandu Kificho akisisitiza yapo baadhi ya mambo ambayo binadamua anaweze kubahatisha la si uendeshaji wa nchi.


Katika mkutano huo mwenyekiti wa mkutano wa bunge maalum alilazimika kutumia mamlaka kwa kushirikiana na mwanasheria mkuu wa serikali kutengua kanuni mara mbili ili kutoa fursa kwa viongozi hao kutoa maoni yao na hatmaye kuliahirisha bunge hilo hadi Agosti 5 mwaka huu.