WATU 6 WAFARIKI KATIKA AJARI NA WENGINE 12 WAJERUHIWA

Watu sita wamepoteza maisha na wengine kumi na mbili wakijeruhiwa kufuatia ajali iliyotokea eneo la Makongo barabara ya Bagamoyo jijini Dar-es-salaam,ikiyahusisha magari manne mawili kati ya hayo yakiwa ni ya abiria maarufu kama Daladala,zifanyazo safari zake kati ya Ubungo,Mwenge,Makumbusho na Tegeta.

Vilio na simanzai vilitawala kwenye maeneo yanayozunguka hosipitali kuu ya jeshi la wanachi wa Tanzania (JWTZ) Lugalo jijini Dar-es-salaam,ambapo mashuhuda wa ajali hiyo wanadai kuwa,dereva aliyekuwa akitokea tegeta kwenda mwenge alikuwa katika mwendo wa kasi ya ajabu.

Mganga mkuu wa hosipitali ya jeshi lugalo iliyopokea majeruhi na maiti hao,Brigedia Jenerali Dkt Makere Josiah, amethibitisha kupokea majeruhi kumi na wawili na maiti sita, huku wengine hali zao zikiwa ni mbaya na kukimbizwa kwenye hosipitali ya taifa ya rufaa Muhimbili kwa matibabu zaidi.