MAUAJI ZAIDI YAWAKUTA WAKAZI MPEKETONI

Picha za kusikitisha za watu waliouawa na kujeruhiwa katika shambulizi lililofanywa MpeketonI Jumapili usiku
Takriban watu 20 wameuawa katika shambulizi la pili la usiku katika pwani ya kenya .
Kundi la wapiganaji la Alshabaab limekiri kutekeleza shambulizi hilo la pili katika vijiji viwili zaidi na kusema kuwa wengi ya waliouwa ni maafisa wa polisi.
Wapiganaji hao walivamia vijiji viwili karibu na mji wa Mpeketoni ,ambao ni eneo la mashambulizi ya kwanza ambayo yalisababisha mauaji ya wau 48.
Hii ni licha ya maafisa wengi wa polisi kupelekwa katika eneo hilo kufuatia mauaji hayo ya Jumapili.
Wakaazi wa eneo hilo wamelalamikia serikali kwa kutowapa ulinzi baada ya shambulizi la kwanza na sasa wanaishi kwa hofu.

Serikali inasema kuwa wanamgambo wa Alshabaab walikata mawasiliano ya simu katika eneo hilo kabla ya kutekeleza shambulizi hilo.
Wanamgambo hao wanaohusishwa na kundi la Alqaeda wanasema kuwa wataendelea kufanya mashambulizi nchini Kenya ikiwa serikali haitaondoa wanajeshi wake nchini Somalia.

Shambulizi hilo la vijijini ni limeonekana kuwa mfumo mpya wa mashambulizi ambayo yamekuwa yakifanya na Al Shabaab ambalo mara nyingi limekuwa likilenga maeneo ya mijini hasa miji mikubwa.
Takriban watu 48 waliuawa katika mashambulizi yaliyofanyika usiku wa kuamkia Jumatatu huku washambuliaji wakishambulia hoteli na kituo cha polisi pamoja na kuteketeza magari.