JAMAA APANDISHWA KIZIMBANI KWA KUFANYA MAPENZI NA MBUZI

MTU mmoja amefikishwa katika mahakama ya wilaya ya Ukerewe, Mwanza kwa tuhuma za kukutwa akifanya mapenzi na mbuzi.

Mtuhumiwa huyo, William Sebastian (21), mkazi wa Kijiji cha Mlezi alisomewa mashtaka hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya wilaya hiyo, Faustine Kishenyi.

Mwendesha Mashitaka wa Polisi, Inspekta Samwel Onyango aliielez amahakama hiyo kuwa mshitakiwa huyo alitenda kosa hilo Juni 4 mwaka huu saa 9 alasiri huko Mlezi, Ukerewe.

Katika hati ya mashitaka imeelezwa kuwa mshitakiwa huyo alikutwa akitenda kosa hilo katika banda la mbuzi nyumbani kwao na mmoja wa wanafamilia.

Katika maelezo hayo, Onyango alisema mwanafamilia huyo ambaye ni mwanafunzi wa darasa la tatu katika Shule ya Msingi Mlezi, baada ya kushuhudia tukio hilo alikwenda kutoa taarifa kwa baba yao, Maxmilian Stephan aliyefika na kumkuta mtuhumiwa akiendelea `kuhangaika' na mbuzi huyo.

Akifafanua, alisema kosa hilo ni kinyume cha sheria ya makosa la kujamiiana kifungu namba K/F 154 (1) na (2) C sura ya 16 ya marekebisho ya sheria ya mwaka 2002. Mtuhumiwa amekana kutenda kosa hilo na amerudishwa rumande kwa kukosa wadhamini.