MTU MMOJA AMEFARIKI NA WENGINE KUJERUHIWA KATIKA SHAMBULIZI LA BOMU ZANZIBAR

Mtu mmoja ameripotiwa kufariki huku wengine kadhaa wakijeruhiwa katika shambulizi la bomu kisiwani Zanzibar.

Baadhi ya waathiriwa walikuwa wanaondoka katikamsikiti mmoja ulioko katika mji mkuu wa Stone Town.

Haijulikani ni nani aliyetekeleza shambulizi hilo ambalo linajiri mkesha wa sherehe za kimataifa za filamu katika kisiwa hicho.

Ni shambulizi la pili la bomu mwaka huu.

Mnamo mwezi February, mabomu mawili tofauti ya kujitengezea yalilipuliwa nje ya kanisa Anglikana mjini Stone Town pamoja na mkahawa uliokuwa karibu na kanisa hilo.

Kumekuwa na hali ya wasiwasi wa kidini katika kisiwa hicho.