FIFA KUMSHITAKI SUAREZ KWA KUMNG'ATA CHIELLINI

FIFA imemshitaki Luis Suarez kwa kumng'ata mlinzi wa Italia Giorgio Chiellini kwenye mechiya Kombe la Dunia, suala ambalo linaweza kumsababishia mchezaji huyo wa Uruguay kufungiwa kucheza mashindano ya kimataifa kwa miaka ipatayo miwili.
Siku ya Jumatano, chombo hicho kinachosimamia mpira wa miguu kilisema kuwa kamati yake ya nidhamu imefungua jalada dhidi ya Suarez, ikiwa ni masaa machache baada ya kuisha kwa mechi mjini Natal.
Maafisa wa Uruguay wameombwa kuwasilisha ushahidi wao saa 2 usiku leo Jumatano.
Suarez, ambaye ameshawahi kusimamishwa mara mbili kwa kung'ata wachezaji, alipigwa picha hivi karibuni akimng'ata Chiellini begani, kabla hajajiangusha chini na kupiga uso wake.
Mwamuzi Marco Rodriguez wa Mexico hakuona tukio hilo na hakufanya chochote.

Hatahivyo, FIFA wana uwezo wa kulishughulikia, "ufunjwaji sheria ambao haukuweza kuonekana kwa maafisa wa michezo", ilieleza taarifa ya FIFA.
Suarez anaweza kufungiwa kwa miaka miwili kama atakutwa nakosa akimshambulia mpinzani.
Uamuzi utatangazwa kabla ya Jumamosi, ambapo Uruguay itacheza na Colombia kwenye hatua ya mtoano kwenye uwanja wa Maracana.