WASAKWA KWA MAUAJI NA KUFUKIA MAITI

KAMANDA wa Polisi Mkoa wa Katavi, Dhahiri Kadavashari, amesema jeshi hilo linawasaka watu watatu kwa tuhuma za kumuua na kumfukia Mbaya Lukondia (36), mwanakijiji wa Kabunde, Kata ya Mamba wilayani Mlele, Mkoa wa Katavi.

Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Ubakila Kidakira, Jimon Dogi 'Lala' na mwingine aliyefahamika kwa jina moja la Omary, wakazi wa Kijiji cha Kabunde.

Kwa mujibu wa Kamanda Kidavashari,kabla ya kifo hicho Lukondia alitoweka nyumbani kwake Aprili mwaka huu hadi Juni 19 mwili wake ulipogundulika ukiwa amefukiwa aridhini huku ukiwa umeharibika.

"Baada ya kufukuliwa na kufanyiwa uchunguzi, ilibainika kwamba kabla ya kufa alipigwa na kitu kizito kichwani na ubavuni… watuhumiwa wa mauaji hayo walikimbia kijijini hapo na mpaka sasa hawajulikani walipo,"

alisema kamanda huyo huku akisisitiza kwamba wanatafutwa kwa kuwa walikimbia baada ya mwili huo kuonekana.


Chanzo: Tanzania Daima