KIKUNDI CHA KATAVI NDIO HOME WATEMBELEA HOSPITALI YA WILAYA YA MAPNDA

Kikundi cha Katavi/Mpanda ndio home kutoka mkoa wa katavi wilayani Mpanda kwa umoja wao ambao pia ni mashabiki wa Manchester United na Arsenal wamefanya jambo la kijamii kwa kutoa msaada kwa wagonjwa katika hospitali ya Wilaya ya Mpanda kwa kuwasaidia maji, Sabuni, Matunda na Biskuti katika wodi tatu za wanawake, mbili za wanaume na moja ya watoto katika Hospitali hiyo.
Picha ya Pamoja Hospitali

   
Abdillazaq na Rajabu Katika Wodi ya Wanawake
 Katika mchakato huo wanakikundi wamejiwekea kila mwaka kutembelea maeneo mbalimbali hususa ni hospitali, magereza na kukutembelea vivutio vya utalii pamoja na kufanya Bonanza la michezo mbalimbali kama mpira wa miguu, kuvuta kamba, kukimbiza kuku na kadharika.

Katika mahojiano ya mtandao huu Katibu wa Kikundi bwana Michael Mazalla na Mwenyekiti Ndugu Dickson Kashura wameeleza kuwa mwaka wa tatu mfululizo sasa Katavi/Mpanda Ndio Home wameweza  kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Katavi, Hospitali ya wilaya Mpanda na kuongeza kuwa katika kuwa karibu zaidi na jamii wamepanga msimu ujao wataweza kutembelea maeneo mengine ikiwamo na Gereza kuu la Mpanda.

Katibu Michael Mazalla akisaini kitabu cha wageni katika Hospitali ya Wilaya

Ndugu Alex SoCksea akimpatia mgonjwa Sabuni.

"Katika kuendeleza utalii wa ndani kikundi kimepanga kutembelea fukwe za ziwa Tanganyika mkoani hapa katika maeneo ya Ikola na Karema mwishoni mwa mwezi June pia katikati ya mwezi July kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Katavi" alisema Katibu
Katibu Michael Mazalla akitoa salam fup kwa wagonjwa katika wodi ya wanawake

Wanakikundi wakielekea katika wodi ya Wanaume
 Katika hari ya kujiweka sawa kimwili wanakikundi walimalizia wikiend kwa mpambano wa mpira wa miguu uliofanyika katika uwanja wa Azimio mjini hapa na Mashabikiwa Manchester united kuibuka na ushindi kwa kuwachabanga wenzao wa Arsenal kwa magoli Manne kwa moja ambapo Mchezaji wa man U Khalid aliweza kufunga goli tatu(Hat trick) peke yake huku lile la kufutia machozi la Arsenal likifungwa na Abdillazaq Osman kwa mkwaju wa penati.
Johnson & Michael

Kikosi cha arsenal kikiongozwa na Kapteni Mike Mertesacker

Kikosi cha Man U kikiongozwa na kapten Hussein  

Picha ya Pamoja
 Mwenyekiti bwana Dickson kashura aliweza kuongelea matitizo yaliyotokea katika kipindi hiki ikiwa ni pamoja na mwanakikundi ndugu Omary Zozi (Picha Chini) kuvunjika mguu eneo la paja baada ya kuanguka mzoezi, pia changamoto nyingine ni uchache wa watu kujitoa katika kutekeleza mkakati wote wa bonanza, akisema kuwa tofauti na mwaka jana ambapo watu walijitokeza kwa wingi.

Omary zozi wkibadilishana mawazo na wanakikundi walipomtembelea.
Kwa upande wa mwanakikundi na Katibu wa kamati ya Usafirishaji bwana Joseph Mtitimya amewataka wananchi wa mkoani hapa kupenda kujitolea na kujumuika na wananchi wengine ilikuweza kusaidiana katika mambo ya kijamii na kiuchumi kwani kwa kujitoa huko kunaongeza upendo, urafiki a undugu kwa ujumla. Aliongeza kwa kuwataka wananchi wa maeneo yote kujitokeza kwa wingi katika safari ya kutembelea maeneo ya Karema, Ikola (Beach) na Katavi National park.
Ndugu frank akigawa sabuni kwa mgonjwa.



Unaweza kuangalia video hapa chini jinsi mchakato mzima ulivyokuwa katika Hospitali ya wilaya ya mpanda.