WANAMGAMBO WATISHIA KUISHAMBULIA BAGHDAD

Wanamgambo wa ISIS wanaotishia kuvamia mji mkuu Baghdad

Wanamgambo wa kiislam ambao wamedhibiti eneo kubwa la Iraq wanasema sasa wataelekeza mashambulio yao katika mji mkuu Baghdad.
Jana kundi lenye uhusiano na mtandao wa al-Qaeda- ISIS liliteka miji ya Mosul na Tikrit, lakini vikosi vya serikali vilitumia mashambulizi ya anga kuzuia wanamgambo hao wasisonge mbele kuelekea katika mji wa Samara.
Lakini mwandishi wa BBC aliye nchini humo anasema vikosi vya serikali vimeonyesha kutokuwa na uwezo wa kukabiliana na mashambuliz na hakuna matumaini ya kurejea kwa hali ya utulivu
Msemaji wa chama cha Dawa cha waziri mkuu wa Iraq kilichopo na makao London, amesema mzozo huo hautosababisha kusambaratika kwa serikali ya Nouri Al Maliki.
Wananchi wengi wamelazimika kutoroka mji wa Mosul hofu ya kushambuliwa

 
 
Zuhair Al Nahar amesema itakabiliana na uhasama wa wapiganaji hao.
Wakati huo huo Uturuki imesema kuwa itafanya mashambulio makali iwapo raia wake wanaozuiliwa na waasi wataumizwa.
Duru za habari zasema kuwa waasi wameuteka ubalozi wa Uturuki, ulioko Mosul na wanawazuia takriban watu 48.
Msemaji katika wizara ya mambo ya nje Marekani, Jen Psaki ameiambia BBC kwamba Marekani ipo tayari kutoa usaidizi.