GAVANA WA LAMU KENYA AKAMATWA



Polisi nchini kenya wamemtia mbaroni gavana wa jimbo la Lamu lililokumbwa na mapigano hivi majuzi na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 65.
Polisi walimshika Issa Timamy,kufuatia tuhuma za kuhusika na mashambulizi yaliyotokea Mpeketoni mapema mwezi huu.
Timamy anatarajiwa kufikishwa mahakamani mjini Mombasa alhamisi.
Punde baada ya tukio hilo rais Uhuru Kenyatta alikatalia mbali madai kuwa ilikuwa shambulizi la kigaidi lililotekelezwa na kundi la waislamu la Al shabab.


Rais Kenyatta alisema kuwa hilo lilikuwa shambulizi lenye misingi ya kikabila na kisiasa.
Kundi la wapiganaji kutoka Somalia Al shabab lilidai kutekeleza shambulizi hilo.
Bwana Timamy ni Gavana wa pekee kutoka chama cha UDF .


Rais Kenyatta alipinga kuhusika kwa Al shabab kwani wengi waliouawa walikuwa wa jamii ya wakikuyu jamii anayotoka rais Kenyatta .
Aidha wavamizi waliwalenga wanaume ambao hawakuwa waislamu na kuwataka kukariri shahada ama aya za Quran,wale walioshindwa walikuawa .
Siku ya jumatano maafisa wa utawala katika jimbo hilo la Lamu walidai kuwa wamewakamata watu 13 waliokuwa wakipanga njama ya kufanya uvamizi zaidi.