VURUGU ZAZUKA WAKIGOMBEA KUZIKA MWILI WA MTOTO

Mtafaruku mkubwa umetoke msibani katika Mtaa wa Kawajense madukani Wilayani Mpanda Mkoa wa Katavi baada ya ndugu wa pande mbili kugombania kuzika mwili wa mtoto aitwaye Junior Bacho mwenye umri wa mwaka mmoja na nusu aliyefariki june 26 majira ya saa saba usiku katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda Tukio hilo la ambalo lilivutia hisia za watu wengi lilitokea hapo juzi katika mtaa huo baada ya marehemu huyo kufariki akiwa amelazwa katika hospitali ya Wilaya ya Mpanda aliko kuwa akiuguzwa na shangazi yake aitwaye Evelyne Komba


Baada ya mtoto huyo kufariki kulitokea kutoelewana baina ya ndugu wa baba wa mtoto aitwaye Joseph Bacho na ndugu wa mama wa marehemu aitwaye Anna Kizo Upande wa ndugu wa baba ulidai wao ndio wenye haki na jukumu la kuchukua mwili wa marehemu na kuupeleka nyumbani kwa mama mzazi wa baba wa marehemu aitwaye Ted Francis (bibi miti) anae ishi katika mtaa wa madukani mjini hapa


Ndugu wa mama wa marehemu nao walidai hawako tayari msiba huo kwenda kwa baba wa marehemu kwani hakuwa na uhalali wakuchua mwili wa marehemu kwa kile walicho dai baba wa marehemu alikuwa ajatowa mahari hivyo wao awamtambui.


Hari hiyo iliwafanya ndugu wa pande hizo mbili kuanza kutupiana shutuma za lawama ambapo ndugu wa baba wa marehemu walimshutumu mama wa marehemu kwa kushindwa kumhudumia marehemu wakati akiwa mgonjwa na muda wote baba wa marehemu alipokuwa akifika nyumbani Anna Kiza alikuwa hamrusu kumwona mwanae kwa kumweleza amelala.


Walidai toka marehemu alipochukuliwa na baba yake hapo june 18 kwa ajili ya kumshughulikia matibabu ya ugonjwa wa ukosefu wa lishe (kashakoo) mama wa marehemu wala ndugu wa upande wake hawakuwahi kufika hata siku moja kumwangalia hari iliyofanya mtoto huyo awe anaangaliwa na shangazi Evelyne yake na bibi yake Ted Pamoja na maelezo hayo ndugu wa mama wa marehemu waliendelea na msimamo wao wa msiba kuwa kwao baada ya mabishano ya muda mrefu pande mbili hizo ziliamua kuuwacha mwili wa marehemu kwenye chumba cha kufidhi maiti katika hospitali ya Wilaya ya Mpanda.

Baaada ya kurudi nyumbani kila upande uliweka msiba nyumbani kwao hali iliyofanya msiba huu kuwe kwa sehemu mbili tofauti katika mtaa mmoja.


Siku iliyofuata wazee wa mtaa huo waliingilia kati mgogoro na kufanya kikao na pande mbili hizo zilizokuwa zikivutana na kufikia uamuzi wa kuwa msiba huo uwe nyumbani kwao na baba wa marehemu Kufuatia uamuzi huo shangazi wa marehemu
Evelyne Komba aliongoza ndugu na kwenda chumba cha kuhifadhi maiti na kuuchukua mwili wa marehemu na kuupeleka kwao na baba wa marehemu kwa ajiri ya maandalizi ya mazishi yaliyokuwa yamepangwa kufanyika juzi saa nane kwenye makaburi ya kawanjense msufini


Wakati huo shughuli za uchimbaji wa kaburi ulifanyika na kaburi lilikamilika ikawa unasubiliwa muda uliopangwa wa kufanyika kwa mazishi.


Baada ya muda mfupi ndugu wa baba wa marehemu walipata taarifa kuwa kaburi walilochimba kwa ajiri ya kumzikia marehemu wameonekana watu wakilifukia hari ambayo iliwafanya waelekee huko makaburini.


Ndugu hao wa baba wa marehemu walipofika makaburini walikuta dada wa mtoto wa marehemu aitwae Jane Kiza na wenzaki wakiwa ndio wanamalizia kufukia kaburi hilo ambalo halikuwa na mwili wa marehemu.

Jane na kundi lake walipoulizwa kwanini wamefukia kaburi hilo walianza kufoka na kisha kundi la ndugu wa mama wa marehemu walitokea hapo na kuanza kuwashambulia kwa kipigo ndugu wa baba wa marehemu.


Askari wa kikosi cha kutuliza ghasia walikuwa wameongozwa na meja wao alijulikana kwa jina la Bahati walifika kwenye eneo hilo na kutuliza ghasia hizo na kisha walielekea eneo la msibani na kuamuru mwili huo wa marehemu urudishwe kwenye chumba cha kuifadhi maiti hadi hapo ufumbuzi wa tatizo hilo utakapo kuwa umekwisha.


Ndugu wa marehemu walikubaliana na uamuzi huo wa kuurudisha mwili wa marehemu kwenye chumba cha kuifadhi maiti.


Chanzo: Katavi yetu