TIGO, ZANTEL NA AIRTEL ZAUNGANA KUBORESHA HUDUMA

Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Airtel Sunil Colaso katikati ni Mkurugenzi Mkuu wa Tigo Diego Gutierrez kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Zantel Pratap Ghose wakiongea na Waandishi juu ya Ushirikiano wao.
Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Airtel Sunil Colaso katikati ni Mkurugenzi Mkuu wa Tigo Diego Gutierrez kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Zantel Pratap Ghose wakiongea na Waandishi juu ya Ushirikiano wao.

Makampuni ya simu za mkononi ya Airtel, Zantel na Tigo nchini Tanzania leo wametangaza kuingia katika ushirikiano wa pamoja ambao utakaowawezesha wateja wao wa Airtel Money, EzyPesa na Tigo Pesa, kutumiana fedha kupitia simu za mkononi, taarifa hiyo ilieleza kuwa huduma hiyo inatarajiwa kuanza mwishoni mwa mwezi huu.
Ushirikiano huo ni wa kwanza na wa aina yake kwa makampuni hayo makubwa ya simu barani Afrika, yanayowawezesha wateja wa kampuni tofauti za simu kuweza kutumiana na kupokea fedha moja kwa moja kwenye akaunti zao za simu tofauti na hapo awali.
Hapo awali kulikuwa na makubaliano ya kupigiana simu na kutumiana ujumbe mfupi wa maandishi, lakini kwa sasa wamesonga mbele zaidi.
Taarifa hiyo inaainisha faida kwa wateja watakazopata kupitia mashirika hayo matatu, kama punguzo la gharama ya kutuma na kupokea simu, pia mteja sasa hatakiwi kuwa na utambulisho wa siri au (PIN CODE) pindi mteja anapotoa pesa zake kama ilivyo sasa.
Wakurugenzi wakuu kutoka makampuni ya Airtel, Tigo na Zantel wakishikina mikono kwa pamoja kuonesha ushirikiano wa kutoa huduma ya kutuma fedha na kutoa fedha.
Wakurugenzi wakuu kutoka makampuni ya Airtel, Tigo na Zantel wakishikina mikono kwa pamoja kuonesha ushirikiano wa kutoa huduma ya kutuma fedha na kutoa fedha.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Airtel Sunil Colaso alisema kuwa, kampuni yake imejikita katika kuwapa wateja wake huduma zenye ubunifu wa hali ya juu bila kujali ushindani wa kibiashara, lengo kuu ni kupata wateja nchi nzima.
Pia Mkurugenzi  Mkuu wa Zantel Pratap Ghose alisema kampuni yake ina dhamira ya dhati katika kuhakikisha thamani na ubunifu wa huduma zake, kwa sababu hiyo kampuni imefurahishwa na ushirikiano huo ambao utawawezesha wateja wote kufanya kazi zao kiufanisi na urahisi zaidi wakiwa sehemu mbalimbali hapa nchini.
Mkurugenzi Mkuu wa Tigo Diego Gutierrez alisema kuwa wanafurahi kushirikiana na makampuni hayo mawili kwa ajili ya kuendeleza huduma ya kutuma fedha na kupokea fedha kupitia simu za mkononi, tunawahakikishia wateja wetu kwamba kadri miamala inavyoongezeka ndivyo na sisi tunazidi kuongeza usalama wa fedha kwa wateja.

Chanzo: Taarifa.co.tz