JWTZ NA POLISI WAFANIKIWA KUHARIBU BOMU

Jeshi la polisi mkoani Mtwara kwa kushirikiana na jeshi la wananchi wa Tanzania wamefanikiwa kuharibu bomu lililokuwa limetelekezwa katika kijiji cha Mdui kata ya Mbawala wilaya ya Mtwara vijijini baada ya kuonekana likichezewa na watoto.

jeshi la polisi mkoani Mtwara kwa kushirikiana na jeshi la wananchi wa Tanzania wamefanikiwa kuharibu mlipuko wa bomu katika kijiji cha Mdui kata ya Mbawala wilaya ya Mtwara vijijini baada ya kuonekana likichezewa na watoto.
Akizungumza na ITV kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Mtwara Maisha Maganga amesema taarifa hizo wamezipata kutoka kwa raia wema baada ya kuonekana likiwa eneo la makaburi.

Amesema baada ya kupata taarifa juu ya bomu hilo lenye kilo nne jeshi hilo lilichukua hatua za haraka ikiwa ni pamoja na kuomba kikosi maalum cha kutegua mabomu kutoka jeshi la wananchi wa Tanzania.
Amesema bomu hilo linaonyesha ni la siku nyingi mahali hapo na liliachwa enzi za vita ya Msumbiji.

Chanzo: ITV