MTU MMOJA AUAWA KWA KUKATWA KATWA KWA SHOKA

Mtu mmoja aliyefahamika kwajina la Charles Mkimbili (60) wa Kijiji cha Kaulolo Tarafa ya Inyonga Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi ameuwa kwa kukatwana shoka kichwanina mtu asiyefahamika wakati akila chakula cha jioni na familia yake.

Tukio hilo la mauwaji ya kinyama lilitokea hapo juzi majira ya saa mbili usiku kijijini hapo nyumbani kwa marehemu Charles Mkimbili Kwa mujibu wa Kamanda wa Jeshi la Polisiwa Mkoa wa Katavi Kamishina Msaidizi Mwandamizi Dhahiri Kidavashari alisema tukio hilo lilitokea nyumbani kwake na marehemu wakati akiwa anakula chakula cha jioni akiwa na familia yake

Alisema wakati marehemu akiwa anakula chakula na familia yake ghafla alitokea mtu mmoja mwanaume akiwa amejifisha sura yake huku akiwa ameshika shoka mkononi

Kamanda Kidavashari alieleza mtu huyo baada ya kuwa kufika hapo walipokuwa wakila chakula alianza kumshambulia marehemu kwa kumkata na shoka kichwani sehemu ya kisogona, usoni huku familia yake ikiwa inapiga matowe ya kuomba msaada kwa majirani

Alisema mtu huyo baada ya kuona mayowe yanazidi aliamua kukimbia na kutokomea mahari kusiko julikana huku akiwa amebeba shoka lake

Alifafanua majirani walifika kwenye eneo hilo na kumkuta marehemu akiwa amegalagala chini huku akiwa tayari ameisha fariki Dunia na pembeni yake damu zikiwa zimetapakaa.

Kamanda Kidavashari alisema chanzo cha mauwaji hayo bado hakijajulikana hivyo Jeshi la Polisi linaendeleana upelelezi wa tukio hilo na kuhakikisha linawatia mbaroni wahusika wa tukio hili ili waweze kufikishwa mahakamani kwa hatua za kisheria.


Chanzo: Katavi yetu