BENKI YA DUNIA YAONYA ONGEZEKO DENI LA TAIFA

BENKI ya Dunia imeonesha wasiwasi kuhusu kuongezeka kwa deni la taifa kutokana na Serikali kuendelea kukopa mikopo ya biashara ya ndani hadi kuzidi kiwango kilichowekwa na Shirika la Fedha Duniani (IMF) kwa asilimia 1.2 ya Pato Halisi la Taifa (GDP).

Hali ya uchumi wa Tanzania iliyotolewa jana na taasisi hiyo, imeonesha nchi imefanya vibaya zaidi katika maeneo ya mauzo ya nje, kushuka kwa nakisi ya fedha yajumla, kushindwa kwa Serikali kukusanya mapato pamoja na ongezeko la ukosefu wa ajira kwa vijana.


Ripoti hiyo iliyobatizwa jina la 'Nanianataka kazi? Nguvu ya Mvutano wa Majiji' imeeleza kuwa Tanzania imeonesha utendaji mbovu zaidi wa mauzo ya nje tangu mwisho wa miaka ya 1990.

Jambo lingine la kutia wasiwasi zaidi ambalo limetajwa na ripoti hiyo ni kwa nakisi ya fedha ya jumla kushuka hadi viwango vilivyosawa na asilimia 6.8 ya GDP katika mwaka 2012/13.

Ripoti hiyo inasema huo ulikuwa niupungufu mkubwa zaidi tangu mdororo wa uchumi wa dunia mwaka 2008/9.


Katika eneo la mikopo, ripoti hiyo ilieleza kuwa thamani ya mikopo ilikuwa juu zaidi kwa asilimia 1.2 ya GDP kuliko lengo lililokubaliwa na Shirika la Fedha Duniani (IMF).

Mikopo hiyo ripoti inaeleza kuwa haikutosha kuziba pengo la fedha kutokana na deni kubwa la nyuma ambayo thamani yake ni karibu asilimia 4 ya GDP hadi ilipofika Juni 2013.


Ripoti hiyo pia imeeleza kuwa roboza mwanzo za mwaka 2013/14 Serikali ilikusanya mapato yake kwa asilimia 82 tu ya lengo la mapato hali iliyosababisha Serikali kupunguza au kuahirisha utekelezaji wa baadhi ya programuza uwekezaji, manunuzi ya bidhaa na huduma.

Pamoja na kuchukuliwa hatua hizo, ripoti imebainisha kuwa thamani ya deni la taifa iliendelea kukua hadi kufikia karibu asilimia 5 ya GDP mwishoni mwa Machi 2014.


Deni hilo halijumuishi malimbikizoya taasisi za Serikali ikiwemo Tanesco na wagavi wake. Ripoti hiyo inasema iwapo madeni hayo yatajumuishwa inaweza kuongeza hesabu ambayo ni sawa na asilimia2 ya GDP kwenye jumla ya thamani ya deni la Serikali.

Uchumi na Ajira Ripoti hiyo imebainisha kuwa idadi ya watu ambao hawana kazi zinazowapatia kipato cha kutosha kuweza kujikimu juu ya mstari wa umasikini inazidi kuongezeka.


"Hatari kubwa ni kwamba wafanyakazi wengi wa mashambaniwanazidi kukimbia kutoka kwenye kilimo kwenda katika biashara za kujikimu zilizoko mijini," inasema ripoti hiyo.

Pia imebainisha kuwa wakati kuna kampuni kubwa zenye mafanikio katika maeneo ya mijini, kiwango kikubwa cha ajira katika maeneo hayo hutolewa na biashara ndogo ndogo zisizokuwa za kilimo ambazohazina tija ambazo zinakosa uwezo wa kupanuka na kuwa shindanishi.


Kuhusu biashara, ripoti ilisema biashara nyingi za mijini ni zile ndogo ndogo ambazo sio rasmi na sio za kitaalamu na huendeshwa nawenye mali ambao wana ujuzi mdogo.

Wamiliki wa biashara hizo, ripoti imewataja kuwa ni wajasiriamali wasio na ari na wanaendesha biashara hizo kwa kuwa tu hawana njia nyingine ya kujikimu kutokana na biashara hizo kutokuwa na faidakubwa.


Pinda azungumza ajira Waziri Mkuu Mizengo Pinda alisema wakati wa uzinduzi wa ripoti hiyo kuwa idadi ya watu wanaoishi mijini inaongezeka hadi kufikia watu milioni 13.3 wengi wao wakiwa vijana ambao wanaenda kusaka ajira.

Pinda alisema hata hivyo vijana hao ambao asilimia 78 hawana elimu yenye ujuzi wanakosa ajira.


Alisema sababu kubwa ya vijana kwenda mijini ni kutokana na kilimo kutowapatia tija hivyo kuamini kuwa mijini kuna maisha mazuri zaidi.

Alisema Serikali inashughulikia tatizo hili la kuhakikisha vijana wanaohitimu shule za msingi na sekondari wanakuwa na ujuzi utakawawezesha kuendesha shughuli halali za kuwapatia kipato.


Alisema licha ya kuwepo vyuo vya ufundi lakini wanafunzi wanaosoma kwenye vyuo hivyo bado ni wachache.

Waziri Mkuu alikiri kuwa takwimu za Ofisi ya Taifa ya Takwimu zinaonesha kuwa jumla ya watu milioni 2.4 hawana ajira na wengi wao ni vijana ambao wamekimbilia mijini.


Alisema Serikali inazo changamoto za kuweka miji yake iweze kukidhi mahitaji ya ajira, lakini akasema bado Serikali inashughulikia suala hilo.

Benki ya Dunia yaasa Mtunzi Mkuu wa ripoti hiyo Jacques Morisset, alisema kuna haja ya haraka kwa Serikali kushughulikia changamoto wanazokabiliana nazo wajasiriamali wadogo katika miji ya Tanzania.


Mkurugenzi wa Benki ya Dunia kwa nchi za Tanzania, Burundi na Uganda, Philippe Dongier alisema licha ya uchumi wa Tanzania kukua;lakini umeshindwa kutengeneza ajira za kutosha zenye tija kwa nguvu kazi inayokua kwa haraka.

"Leo hii kuna Watanzania milioni 23 ambao wako katika soko la ajira, watafikia milioni 45 ifikapo mwaka 2030 wakiwa na matumainimakubwa ya kazi zenye heshima na maisha mazuri," alisema Dongier.


Chanzo: Habari Leo