HAKIMU ALIYEMHUKUMU SADDAM KUNYONGWA NAE ANYONGWA

Hakimu ambaye alimhukumu kifo kiongozi wa zamani wa Iraq Saddam Hussein amekamatwa na kunyongwa na wanamgambo wa ISIS, inadaiwa hivyo.


Raouf Abdul Rahman, ambaye alimhukumu kifo dikteta huyo kwa kunyongwa mwaka 2006, aliripotiwa kuuawa na waasi kwa kulipiza kisasi kwa kuhukumu kunyongwa kwa kiongozi huyo aliyekuwa na umri wa miaka 69.

Kifo chake hakijathibitishwa na serikali ya Iraq, ila maafisa hawajakataa taarifa za kuhusu kukamatwa kwake na waasi wiki iliyopita.

Anaaminikia kuwa alikamatwa Juni 16, na kuuawa siku mbili baadae.

Mbunge wa Jordan Khalil Attieh aliandika kwenye ukurasa wakewa Facebook kwamba Hakimu Rahman, ambaye aliiongoza Mahakama ya Jinai wakati wa kesi ya Saddam, alikamatwa na kuhukumiwa kifo.


"Wanamapinduzi wa Iraq walimkamata na kumhukumu kifo kwa kile kinachodaiwa kulipiza kisasi kutokana na kifo cha Saddam Hussein", alisema, kulingana na Al-Mesyroon.

Attieh pia alisema kwamba Jaji Rahman alishindwa kutoroka Baghdad akiwa amevaa nguo zamcheza muziki.