VURUGU ZAZUKA BAADA YA WAZAZI KUKATAA MAITI YA MTOTO WAO

Vurugu kubwa zimetokea katika kijiji cha Buyango wilayani Muleba mkoani Kagera baada ya wazazi kuikataa maiti ya mtoto wao kwa madai amenyofolewa viungo vyake vya mwili hali iliyosababisha polisi kutumia mabomu ya machozi kutawanya makundi yaliyofunga barabara na kubomoa chumba cha kuhifadhia maiti kutafuta viungo hivyo.


Vurugu hizo zimetokea baada ya mama mmoja mkazi wa Arusha aliyepeleka maiti ya mtumishi wake wa ndani na kuwakabidhi wazazi wake kwa mashariti ya kutoifunua hali iliyosababisha mtafaruku mkubwa ambapo mama huyo amelazika kwenda hospitali kukabidhi mwili huo ambapo baadhi ya ndugu na jamaa walivamia chumba cha kuhifadhi maiti na kubomoa mlango kisha waka angalia mwili ambao wameukuta ukiwa na majeraha na kwamba haufanani na binti yao aliyefahamika kwa jina la Ajela Tilifon mwenye umri wa miaka 16 aliyechukuliwa kijijini hapo tangu mwaka 2012 kwa lengo la kwenda kufanya kazi za ndani mjini Arusha na kwamba baada ya ndugu kukataa kupokea mwili askari polisi wamewakamata ndugu na mwaandishi wa habari kwa madai kuwa wanahamasisha vurugu.


Kufatia hali hiyo mkuu wa wilaya ya Muleba Bw. Lebris Kipuyo alilazimika kufika eneo la vurugu na kuamuru askari polisi kutawanya wananchi ili magari yaweze kupita na baadaye alifika hospitali na kuteuwa baadhi ya ndugu, jamaa na wazazi wa mtoto ambao walikagua mwili wa marehem kisha mkuu wa wilaya akawahutubia wananchi na kuwata ka walioshuhudia mwili waseme ukweli walichokiona nao bila kusita wamesema maiti inamaj raha tumbo limetobolewa na sehem za mwili zimekwaruzika kisha akavishwa nguo na soksi ili kuficha ukweli.


Naye mwaandishi wa habari wa kujitegemea gazeti la Mwananchi aliyejeruhiwa na askari polisi kwa kupigwa virungu Bw. Shaban Ndyamkama amesema kuwa yeye ndiye aliyetoa taarifa za vurugu hizo kwa mkuu wa wilaya ya Muleba baada ya askari kufika eneo la tukio walimkamata na kumshambulia kwa vipigo kisha wakamshikiria kwa muda hadi wananchi waliposhinikiza kuachiwa kwake na baada ya waandishi wa ITV, Radio one kanda ya ziwa kumuomba kamanda wa polisi mkoa wa Kagera Bw. George Mayunga ambaye amekili kwa njia ya simu kuwa vurugu hizo zimesababisha uvunjifu wa amani na kumtaka mkuu wa polisi wilaya ya Muleba kumuachia huru mwaandishi wa habari ambaye amepelekwa hospitali na wananchi kwa matibabu zaidi.