MRAMBA APUNGUZA SHAHIDI MMOJA

WAZIRI wa Fedha wa zamani, Basil Mramba, anayekabiliwa na kesiya matumizi mabaya ya madaraka na kusababisha hasara yash bilioni 11.7, ameiambia Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, kuwa anamuondoa shahidi wake wa tatu ambaye alikuwa ni Naibu Kamishna wa Income Tax, Felisian Busigala (67), katika orodha yamashahidi ambao awali alikuwa anataka wamtetee.

Kesi hiyo jana ilikuja kwa ajili ya jopo la majaji watatu, John Utamwa, Sam Rumanyika na Sauli Kinemela kutoa uamuzi wa pingamizi lililowasilishwa na upande wa jamhuri ambalo liliomba mahakama hiyo, imuondoe Busilaga katika orodha ya mashahidi wa Mramba.


Hatua hiyo ni kutokana na ushahidi alioanza kuutoa Septemba 20, mwaka2013, kuonyesha amefika mahakamani hapo kama mtaalamu wa masuala ya kodi na siyo shahidi ambaye anastahili kuzungumzia mashitaka yanayomkabili Mramba.


Wakili wa Mramba, aliwasilisha ombi hilola kuomba mahakama imuondoe shahidi huyo katika orodha yamashahidi, ombi ambalo lilikubaliwa na Jaji Utamwa, na wakili Swai aliomba kesi hiyo ihairishwe hadi Agosti 21, mwaka huu.

Alisema sababu ya kufanya hivyo ni kutokuwapo na shahidi, ombi ambalo lilikubaliwa na jopo hilo.


Septemba 20, mwakajana, mawakili wa serikali waandamizi; Shadrack Kimaro na Oswald Tibabyekomya, waliweka pingamizi hilo wakiomba shahidi huyo asiendelee kutoa ushahidi wake kwa sababu alionyesha kuwa alifika mahakamani hapo kutoa ushahidi wa kitaalamu na sio wa mashitaka yanayomkabili Mramba.

Mapema jana, Busigala akiwa kizimbani alijibu maswali ya wakili Nyange ambayo yalimtaka afafanue maana ya 'Net of all taxes' kwa sababu kwamujibu wa mkataba ulioingiwa na Benki Kuu na Kampuni ya Alex Stewart inaonyesha benki hiyo kwa niaba ya serikali iliridhia kampuni hiyo ichukue asilimia 1.9 ya dhahabu yote atakayokuwa ameishaikagua.


Busigala alianza kufafanua kuwa 'Net of all taxes' katika mkataba ule maana yake Kampuni ya Alex Stewart itaondoka na asilimia 1.9 baada ya kumaliza ukaguzi wa dhahabu na hiyo asilimia 1.9 ni baada ya kodi yote kukatwa na serikali na kwamba kama kisinge kuwepo hicho kipengele kwenye ule mkataba, ni kwamba Kampuni ya Alex Stewart ingelipwa fedha zaidi na serikali ili mwisho wa siku kampuni hiyo iweze kulipa kodi husika kwa serikali.


Kwamba tatizo hapo siku zote kodi zimekuwa zikibadilika kwani zinapanda na kushuka na hivyo ingelikuwa ni vigumu kwa serikali kuweza kutekeleza matakwa ya mkataba ambao usingekuwa na kipengele hicho cha kumlipa moja kwa fedha kampuni na kisha kampuni ije ilipe kodi husika kwa serikali.


Maelezo hayo ndiyo yalisababisha mawakili wa upande wa jamhuri kuwasilisha pingamizihilo ambalo lilisababisha mahakama kumtaka shahidi huyo asindelee kutoa ushahidi wake hadi watakaposikiliza pingamizi hilo kwa njia ya maandishi na watalitolea uamuzi Oktoba 25, mwaka huu.


Novemba 2008 ilidaiwa mahakamani hapo kuwa Mramba na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Daniel Yona na Katibu Mkuu mstaafu wa Wizara ya Mipango naUchumi, Gray Mgonja wanakabiliwa na makosa mbalimbali ya matumizi mabaya na kuisababishia serikali hasara ya sh bilioni 11.7.