WAZIRI MKUU AWASILI MKOANI KATAVI KWA MAPUMZIKO YA CHRISTIMAS

Waziri Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda jana mchana aliwasiri mkoani Katavi kwa ajiri ya mapumziko ya Krismasi na mwaka mpya na kupokewa na mamia ya wakazi wa mji wa Mpanda waliongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dokta Rajabu Rutengwe kwenye uwanja wa ndege wa Mpanda Waziri Mkuu Pinda aliwasiri kwenye uwanja wa ndege wa Mpanda majira ya saa nane na nusu mchana na kisha alikagua vikundi mbalimbali vya ngoma ya asili akiwa amefuatana na Balozi wa China Nchini Tanzania Baada ya kugagua vikundi hivyo vya ngoma Waziri Mkuu Pinda alielekea kijijini kwake kata ya Kibaoni kwa ajiri ya mapumziko ya Krismasi na mwaka mpya.

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi siku ya jumanne ya tarehe 24 Desemba 2013.

Waziri Mkuu Pinda atatembelea na kukagua barabara inayojengwa kwa kiwango cha rami kutoka Mpalamawe Wilaya ya Nkasi Mkoa wa Rukwa hadi Kibaoni Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi.

Waziri Mkuu Pinda katika ukaguzi huo wa barabara ya Mpalamawe Kibaoni atakuwa ameongozana na Balozi wa China Nchini Tanzania ambapo barabara hiyo inajengwa na kampuni ya kutoka chIna