MECHI YA STARS NA KENYA YAHAMISHWA

TANZANIA VS KENYA SASA SAA MOJA:

Mechi ya Kili Starsvs Kenya ya Kombe la Chalenji iliyopaswa kuchezwa saa 7 na nusu mchana huu Uwanja wa Kenyatta, Machakos imehamishiwa Nyayo, Nairobi kutokana na uwanja kufurika.Kocha Kim Poulsen wa Kili Star s, ambao walikuwa wa kwanza kufika Kenyatta, alilalamikia ubovu wa uwanja huo toka mapema, akiwaambia viongozi wa Shirikisho la Soka Kenya kuwa haustahili kutumika kwa mechi za kimataifa kwa viwango vya Fifa.

Mwandishi wetu toka Machakos anatuambia kuwa pamoja na jitihada za vigogo wa Soka wa Kenya kutaka kulazimisha mechi hiyo ichezwe Kenyatta mchana huu, viongozi wa timu pande zote mbili walikubaliana kwamba hali yauwanja hairuhusu kandanda hilo kuendelea kwani nyasi zimejaa maji kiasi kwamba mpira hata kudunda hauwezi.

Hadi saa nane hii, tunaambiwa wachezaji wa Tanzania wameshaondoka Machakos wakielekea Nairobi kujiandaa na mechi jioni, huku wenzano wa Kenya wakibaki wanashangaa-shangaa hapo Kenyatta Stadium


Chanzo: Mwanaspoti-fb