ABU QATADA AKANA MASHTAKA YA UGAIDI

Mhubiri matata wa kidini, Abu Qatada amekana mashtaka ya ugaidi yanayomkabili aliposomewa katika mahakama moja nchini Jordan.

Mtuhumiwa huyo Mpalestina, Mjordan alihukumiwa bila kuwepo mahakamani kwa kuhusika na shambulio la kigaidi la mwaka 1998 na kula njama ya kufanya shambuliola kigaidi mwaka 2000, lakini sasa amesomewa upya makosa hayo.

Jitihada zake za miaka minane kutaka kubakia Uingereza, zilimalizika mwezi Julai mwaka huu aliporejeshwa nchini Jordan ili akakabiliane na mashitaka hayo.

Ameiambia mahakama kuwa Jordanimevunja makubaliano na Uingereza kwamba angepewa nafuukatika mashitaka yake kwa sababu mmoja wa majaji walioteuliwa kusikiliza kesi hiyo ni kutoka jeshini. "mahakama imekiuka masharti yaliyonifikisha hapa," amesema.

"nataka haki yangu- Siitambui mahakama hii.

"'msingi wa kukiuka mkataba'Wakati Abu Qatada akipinga kuondolewa nchini Uingereza, serikali ya Jordan aliwahahakikishia mawaziri kuwa kesi yake ingesikilizwa na majaji wa kiraia pekee.

Japokuwa Abu Qatada alihukumiwa kifungo cha maisha siku za nyuma bila kuwepo mahakamani, lakini kwa mujibu wa sheria za Jordan anaweza kushitakiwa upya kwa makosa hayo akiwepo mahakamani.

Abu Qatada alipewa hifadhi ya ukimbizi nchini Uingereza mwaka 1994 lakini alipogundulika kuwa msimamo wake unazidi kuwa mkali, vyombo vya usalama vilimwona kuwa mtu hatari na kutakiwa kuondolewa nchini humo.