MTU MMOJA AFARIKI NA WENGINE 19 WAJERUHIWA BAADA YA BUS KUPATA AJARI

Mtu mmoja Beritine Batazal 42 Mkazi wa Kijiji cha Mwese Wilaya ya Mpanda amekufa baada ya basi dogo alilokuwa akisafiria kupinduka baada ya kuacha njia na kusababisha watu wengine 19 kupata majeruhi na kulazwa Hospital.

Kwa mujibu wa Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Katavi Kamishina Dhahiri Kidavashari ajari hiyo ilihusisha basi dogo aina ya Hino lenye namba za usajiri T 894 APW lililokuwa likiendeshwa na mmiiliki wa gari hilo Dickson Kinyonto ambae alitoroka baada ya kutokea tukio Kidavashari alieleza ajali hiyo ilitokea hapo Desemba 16 majira ya saa sita na nusu mchana katika eneo la Ilembo umbali wa kilimeta tatu kutoka Mpanda mjini barabara ya Mpanda ya kwenda Sumbawanga Mkoa wa Rukwa.

Alisema gari hilo ambalo lilikuwa litikokea Tarafa ya Mpimbwe Wilaya yaMlele likielekea Mpanda mjini lilipata ajali hiyo baada ya taili lambele la upande wa kushoto kupasuka na ndipo lilipoacha njia na kupinduka na kusababisha kifo cha Beritine na majeruhi 19 ambao wamelazwa katika Hospitali ya wilaya ya Mpanda na watatu kati yao hari zao sio nzuri.

Kamanda Kidavashari aliwataja majeruhi hao kuwa ni Charles Sokoni 25 mkazi wa mtaa wa Nsemlwa mjini Mpanda ,George Sengeka 48 mkazi wa Mpimbwe, January Damiano 38 mkazi wa mtaa wa Kasimba Ezekiel Benjamin 44 mkazi wa Kashaulili Mpuluku Magobo mkazi wa Ikingwa Saimoni Bala 25 Mkazi wa kata ya KibaoniMajeruhi wengine ni Paul Clement 28 mkazi wa kijiji cha Tinde Lyoba Mengo 36mkazi wa Majimoto E 3170 CPL Albano polisi wa kituo cha Kibaoni Selemani Njala 62 mkazi wa kijiji cha Sosayati Magret Cosmas 29Usinge Justine Michael 17 Bariadi Shinyanga , Cristina Gabriel 60 Stalike Mlele , na Kabura Sahani Majimoto Mpimbwe.

Kidavashari alisema majeruhi wote wanaendelea kupatiwa matibabu kwenye Hospitali ya Wilaya ya Mpanda na mwili wa marehemu Beritine wamekabidhiwa ndugu zake kwa ajali ya mazishi yatakayofanyika kesho kijijini kwao mwese.

Jeshi la polisi linaendelea kumtafuta mtumiwa dereva wa gari hilo Dickson Kinyonto ambae alitoroka baada ya Tukio ili aweze kufukishwa mahakamani kujibu tuhuma za kusababisha ajali.