KENYA WAZIMA MITAMBO YA ANALOGIA

Vituo vitatu vikubwa vya televisheni nchini Kenya vimezima mitambo yao baada ya Mahakama Kuu nchini humo kutoa uamuzi kwamba vinapaswa kuingia katika mfumo wa utangazaji wa dijitali na kuachana na mfumo wa analojia.

Vituo hivyo vya Standard Group, Nation Media Group na Royal Media Services, awali vilikwenda mahakamani kuomba kuahirishwa muda wa kuhamia kwenye mfumo huo, hadi masuala kadhaa yatakapofafanuliwa