ABILIA WANUSURIKA KUFA BAADA YA NDEGE KUPASUKA MATAIRI, BAADHI MAJERUHI WA AJARI YA BASI WARUHUSIWA

ABIRIA kadhaa akiwemo Waziri Mkuu wa zamani ambaye kwa sasa ni Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, wamenusurika kufa baadaya ndege waliyokuwa wakisafiria kupasuka matairi yote manne ya nyuma wakati ilipokuwa ikitua katika Uwanja wa Ndege wa Arushauliopo eneo la Kisongo, jana mchana.

Ndege hiyo ya shirika la ndege la Precision aina ya ATR yenye namba PW 0422 ilipata ajali hiyo wakati ikitua. Kutokea kwa ajali hiyo kumethibitishwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas aliyesema ndege hiyo ilikuwa ikitokea Dar es Salaam kwenda Arusha.

Kamanda Sabas alisema ajali hiyo ilitokea majira ya saa 7 mchana baada ya matairi yake manne ya nyuma kupasuka wakati ikitua katika uwanja mdogo wa ndege wa Kilimo Anga Arusha. "Ajali imetokea majira ya saa saba mchana lakini hakuna mtu yeyote aliyepoteza maisha wala kujeruhiwa katika ajali hiyo kwa kuwa ilitua salama," alisema.

Alisema mpaka hivi sasa ndege hiyo ipo katika uwanja huo huku wataalamu mbalimbali wakiendelea na uchunguzi wa tukio hilo ili kubaini sababu ya ndege hiyo kupasuka magurudumu yake yote manne ya nyuma.

Hata hivyo, Kamanda Sabas alisema uchunguzi wa awali unaonesha kuwa huenda sababu kubwa ya kupasuka kwa magurudumu hayo ni kutokana na matope yaliyokuwepo katika njia ya kukimbilia ndege kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha mkoani hapa.

Alisema kwa taarifa hizo za awali alizonazo, hakuweza kupata nambaya ndege hiyo iliyopata ajali wala idadi ya abiria wake kwa kuwa alikuwa nje ya ofisi yake na kuahidikuitolea ufafanuzi zaidi atakaporejea ofisini.

Majeruhi ajali ya Tanga Wakati hayo yakitokea Arusha, kutoka Tanga Mwandishi Wetu Anna Makange anaripoti kuwa, majeruhi 35 kati ya 93 walionusurika kifo katika ajali ya basi la Kampuni ya Burudani linalosafiri kati ya Korogwe na Dar es Salaam, wameruhusiwa kurudi nyumbani baada ya kupatiwa matibabu na hali ya afya zao kuonekana inaendelea vizuri.

Majeruhi hao ni wale waliopokelewa juzi kwenye Hospitali ya Magunga iliyoko wilayani Korogwe kutoka kijiji cha Kwalaguru kilichopo wilayani Handeni eneo ilikotokea ajali hiyo iliyosababisha abiria wengine 12 kupoteza maisha papo hapo akiwemo dereva wa basi hilo, Luta Mpenda.

Miili ya marehemu hao iliyokuwa imehifadhiwa katika chumba cha maiti cha hospitali ya Magunga hadi jana mchana tayari ilikuwa imetambuliwa na kuchukuliwa na familia zao kwa ajili ya shughuli za maziko zilizofanyika katika maeneotofauti ya wilaya hiyo ya Korogwe.

Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Magunga, Dk Aedes John amethibitisha kuruhusiwa kwamajeruhi hao alipozungumza katika mahojiano na wanahabari hospitalini hapo jana mchana.

Alisema majeruhi wengine 15 wamelazimika kuwahamishia katika Hospitali za Rufaa za Bombo(Tanga), KCMC (Moshi) na Taasisi yaMifupa na Mishipa ya Fahamu ya Muhimbili (MOI) kutokana na kupata majeraha makubwa yaliyosababishwa na kuvunjika kwa viungo ikiwemo miguu, mikono na kifua pamoja na kuvuja damu kwa wingi. "Kati ya majeruhi hao tuliowapa rufaa yumo mtoto mdogo mmoja, wanawake wanne pamoja na wanaume 10 na kwamba kati yao waliopelekwa MOI ni watano, hospitali ya Bombo mmoja, majeruhi kumi walihamishiwa KCMC," alisema.Aidha, alibainisha kwamba kuhusu majeruhi wengine waliosalia akiwemo mtoto mmoja wanawake 15 pamoja na wanaume tisa ambao bado wamelazwa katika hospitali hiyo ya Magunga hali ya afya zao imeendelea kuimarika.

Katika hatua nyingine, baadhi ya wakazi wa Mkoani Tanga waliozungumzia kwa nyakati tofautitukio la ajali hiyo walimtaka Kamanda wa Polisi mkoa wa Tanga,Costantine Massawe kuwawajibisha askari wa usalama barabarani waliokuwa zamu jana katika vituo vya ukaguzi vya askari barabarani vilivyopo kati ya Korogwe na eneo la ajali, kwani waliruhusu basi hilo kuendelea na safari licha ya kujaza abiria kupitia kiasi.

Simiyu Express nalo laua Mwandishi wetu Sifa Lubasi kutoka Dodoma anaripoti kuwa, siku moja baada ya ajali ya basi la Burudani mkoani Tanga, basi jingine la Simiyu Express limeua abiria wawili na kujeruhi wengine 14 baada ya basi hilo kupinduka katikaeneo la Ihumwa nje kidogo ya Manispaa ya Dodoma.

Basi hilo lenye namba za usajili T 717 ANL aina ya Scania lilikuwa likiendeshwa na dereva aliyetambulika kwa jina la MrambaIssa (31).

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani hapa Susan Kaganda, alisema kuwa basi hilo lilikuwa linatokea Bariadi kwenda Dar es Salaam likiwa na abiria 60 liliacha njia na kupinduka kutokana na mwendo kasi.

Kamanda alisema kwamba ajali hiyo ilitokea jana alfajiri majira ya saa tisa katika barabara ya Dodoma-Dar es Salaam eneo la Elshadai. Kamanda Kaganda aliwataja waliofariki katika ajali hiyo kuwa ni pamoja na dereva wa basi hilo Mramba Issa mkazi wa Magomeni, Dar es Salaam na FloraErnest (21) Mwalimu wa shule ya msingi Mwamoto Kolokolo, Bariadi.

Aidha kamanda akizungumzia zaidi ajali hiyo alisema kwamba basi hilolilikuwa likiwakwepa askari wa barabarani kwa kupita njia za panya.

Alifafanua kuwa kwa basi hilo kusafiri usiku huo ni kukwepa askari.

Aliwataka pia wamiliki wa magari kuweka madereva wawili kwa magari ya masafa marefu na pia wazingatie sheria za barabarani.


Chanzo: Habari leo