RASIMU YA PILI YA KATIBA MPYA KUKABIDHIWA KWA RAIS 30 DECEMBER

RAIS Jakaya Kikwete, Desemba 30 atakabidhiwa Rasimu ya Katiba mpya, baada ya kufanyiwa marekebisho na Tume ya Mabadiliko ya Katiba Mpya.

Makabidhiano hayo yatafanyika katika viwanja vya Karimjee, jijini Dar es Salaam, mbele ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohammed Shein, kuashiria kuanza kwa hatua inayofuata ya uundaji wa Bunge Maalumu la Katiba.

Taarifa ya Katibu wa Tume, Assaa Rashid, iliyotumwa jana kwa vyombo vya habari, ilifafanua kwamba mbali na Dk Shein, makabidhiano hayo yanatarajiwa kushuhudiwa na viongozi wengine wa Serikali, vyama vya siasa, taasisiza dini, asasi za kiraia na wananchi wa kawaida.

Awali Rasimu hiyo ilitarajiwa kukamilika kabla ya Desemba 15 baada ya kuongezwa muda na Rais kwa mara ya kwanza, lakini Tume iliomba kuongezwa muda wa kukabidhi Rasimu hiyo kwa mara ya pili na kuongezwa siku 14 kuanzia Desemba 16.Kwa hatua hiyo, Rais Kikwete alikuwa ameiongeza muda Tume hiyo kwa siku 59, kati ya siku 60 ambazo anaruhusiwa kuongeza kisheria.

Bunge la Katiba Kwa mujibu wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba wa Mwaka 2013, baada ya Rasimu hiyo kukabidhiwa, Tume itavunjwa ili kutoa nafasi kwa uundwaji wa Bunge Maalumu la Katiba.

Bunge hilo litaundwa na wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambao ni 357, wajumbe wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar 76 na wajumbe wengine 201 watakaoteuliwa na Rais kutoka mashirika yasiyo ya Serikali na taasisi za kidini.

Mashirika yasiyo ya Serikali na taasisi za kidini, yatatakiwa kupendekeza majina ya watu wanne hadi tisa, ambayo yatapelekwa kwa Rais, naye atateua majina matatu.Rais kabla ya uteuzi huo, atakaa na vyombo vyake na kuteua majina yawajumbe ndani ya mapendekezo ya mashirika na taasisi hizo.

Uamuzi wa vipengele vya Katiba mpya ndani ya Bunge hilo, unatarajiwa kufanyika kwa kupigiwa kura ambapo kila kipengele kitapita kwa kupata kura ya zaidi ya theluthi mbili ya wajumbe kutoka Tanzania Bara na Zanzibar, na hivyo kutoa Rasimu yatatu ya Katiba ambayo itapelekwa kwa wananchi.

Kura ya maoni Baada ya Bunge Maalumu la Katiba, kukamilisha kutengeneza Rasimu ya tatu ya Katiba, makundi ya watu, vyama naasasi za kiraia wanaokusudia kupinga na kuunga mkono Rasimu hiyo yataundwa katika kamati na kusajiliwa katika majimbo.

Tume ya Uchaguzi Tanzania (NEC) na Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), ndizo zitakazo wajibika katika kusajili kamati hizo katika majimbohusika.

Kamati hizo zitateua mawakala wa kusimamia kura zitakazokataa au kukubali Katiba mpya, ambazo zitapigwa na wananchi.

Upigaji kura Katika upigaji kura ya maoni kwa ajili ya upatikanaji wa Katiba mpya, kutakuwa na maswali, likiwamo la wapigakura kutakiwa kujibu ndiyo, kwamba wanaikubali Katiba mpya au hapana, kwamba wanaikataa.

Swali hilo la kura ya maoni litaandaliwa na NEC na ZEC na litahitaji jibu la ndiyo au hapana, tofauti na utaratibu wa uchaguzi uliozoeleka wa kupigia kura mtu auchama.

Aidha, NEC na ZEC ndizo zilizopewawajibu kisheria wa kusimamia uendeshaji wa kura ya maoni na kusimamia elimu ya wapiga kura ya maoni.

Tume hizo pia ndizo zitateua wasimamizi wa kura ya maoni wa kila jimbo kusimamia uendeshaji wa kura ambapo kila msimamizi kwa kushirikiana na tume zote mbili, atateua maofisa na naibu maofisa wa kura ya maoni kwa ajiliya kusimamia vituo vya kupigia kura.

Wapiga kura watakuwa waliosajiliwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga kura la NEC na ZEC.

Hivyo kila mwananchi mwenye sifana aliyeandikishwa kwenye madaftari hayo ya kupiga kura, atashiriki kura ya maoni.