KILLI STARS WAUWA WAGANDA HUKU IVO MAPUNDA AKIIBUKA SHUJAA

Ivo Mapunda ameibuka shujaa wakati Kilimanjaro Stars ikitinga nusu fainali ya michuano ya CECAFA katika mchezo uliofanyika jijini Mombasa.

Uganda walikuwa wa kwanza kuliona lango la Stars katika dakika ya 16 kupitia kwa Dani Sserunkuma huku Stars ikichachamaa na kusawazisha kupitia kwa Mrisho Ngassa katika dakika ya 18. Ilikuwa ni Ngassa alieziona nyavu za Uganda kwa mpira ya adhabu ndogo baada ya Mbwana Samatta kufanyiwa madhambi na kufanya hadi mapumziko Stars wawe mbele kwa2-1.

Kipindi cha pili Stars ilipata pigo baada ya Salum Abubakar kuonyeshwa kadi nyekundu katika dakika ya 53 na kufanya Stars icheze kipindi kikubwa cha pili ikiwa pungufu.

Katika dakika ya 73 Uganda walisawazisha kupitia kwa Martin Mpuga na kufanya dakika 90 za mchezo zimalizike matokeo yakiwa 2-2 na kulazimika kwenda kwenye mikwaju ya penati.

Kevin Yondan, Athumani Iddi na Amri Kiemba walifunga kwa upande huku Mbwana Samatta na Erasto Nyoni wakikosa na Ivo Mapunda kupangua mikwaju miwili ya penatina kuipeleka Stars nusu fainali.

HONGERA SANA Kilimanjaro Stars.