ABIRIA 200 WANUSURIKA KIFO

Abiria zaidi ya 200 waliokuwa wakisafiri na ndege ya shirika la ndege la Ethiopian airline iliyokuwa inatoka Adiss Ababa nchini Ethiopia kwenda uwanja wa ndege wa Kilimanjaro wamenusurika kufa baada ya ndege hiyo kutua katika uwanja mdogo wa ndege wa Arusha na kuserereka hadi pembezoni mwa uwanja huo.

Ndege hiyo aina ya Boing 767 yenye uwezo wa kubeba abiria 300 ilikuwa na abiria 213 na wahudumu 23 na ilitua katika uwanja huo majira ya sita mchana baada ya kushindwa kutua katika uwanja wa ndege wa kilimanjaro kwa sababu ambazo hazikuweza kufahamika mara moja.

Baadhi ya viongozi na akiwemo mkuu wa mkoa wa Arusha Magesa Mulongo na baadhi ya watendaji wa sekta ya usafiri wa anga wamesema sababu zandege hiyo kutua katika uwanja wa Arusha badala ya uwanja wa KIA bado hazijajulikana lakini wamethibitisha kuwa abiria wotewako salama.

Pamoja na viongozi na watendajiwa sekta mbalimbali kuwasili katika uwanja huo abiria waliokuwa katika ndege hiyo waliendelea kukaa ndani ya ndege kwa zaidi ya masaa matano kwa kile kilichodaiwa kuwa ni kukosekana kwa ngazi inayoweza kutumika kuwashusha abiria hao na mwishowe walilazimika kushushwa kwa utaratibu usio rasmi.

Wakizungumza baada ya kushushwa kwenye ndege na kupakiwa kwenye magari hayo baadhi ya abiria wamesema walianza kusikia mtikisiko mkubwa kabla ya ndege hiyo.