MTOTO WA MANDELA AELEZEA SIKU ZA MWISHO ZA BABA YAKE

Huku bunge la afrika kusini likifanyakikao maalum cha kumheshimu mandela ,mwanawe mkubwa wa kike Makaziwe ameiambia BBC kuhusu siku za mwisho za maisha yababaake.

Amesema kuwa ijapokuwa hakuwa akifungua macho mara kwa mara, alikuwa na uhakika kuwa aliweza kusikia vile familia yake ilivyompenda.

Makaziwe amekiri kuwa hakuweza kuwasiliana vyema sana na babake na kwamba babaake hakuweza kuonyesha hisia zake,lakini yote hayo alitaka familia yake kupatana.

Amesema kitu kikubwa alichoelimishwa na babaake ni kuwana ujasiri wa kusamehe.