JESHI LA POLISI LAONYA UPIGAJI FATAKI NA BARUTI

Jeshi la polisi katika kanda maalum ya Dar es Salaam limepiga marufuku ulipuaji wa mafataki kwa mtu ama taasisi yoyote katika mkesha wa mwaka mpya kutokana na kuwepo tishio la vitendo cha kigaidi katika nchi za Afrika ya mashariki.

Kamishina wa kanda hiyo Suleiman Kova amesema wameamua kufanya hivyo ili kuzuia fursa kwa magaidi kutumia uwepo wa milio ya mafataki na wao kulipua mabomu.