SERIKALI YA SUDAN KUSINI YAJARIBU KUTWAA MAJIMBO YALIYOCHUKULIWA NA WAASI

Serikali ya Sudan Kusini imejaribu leo kuyatwaa tena majimbo mawili yaliyochukuliwa na wanajeshi waasi wanao mtii makamu wa rais wa zamani, Riek Machar, huku mapigano katika taifa hilo changa, yakiwa yameingia wiki yake ya pili.

Wakati huo huo, Rais wa Marekani, Barack Obama ameahidi kuchukua hatua zaidi iwapo itahitajika.

Kwa upande wake Umoja wa Mataifa umeahidi kupeleka vikosi zaidi vya kulinda amani Sudan Kusini