LIVERPOOL WAMUANDALIA SUAREZ MKATABA MNONO

Klabu ya Liverpool imeanza mazungumzo na wakala wa Luis Suarez kuhusu mkataba mpya ambao utamfanya mshambuliaji huyu wa Uruguay kua mchezajji mwenye mshahara mkubwa kupita wote katika historia ya klabu hiyo.

Mkurugenzi mkuu Ian Ayre alirejea Liverpool kutoka Uhispania siju ya Jumaanne baada ya kufnya mazungumzo na wakala wa Suarez, Pere Guardiola.

Wamiliki wa Liverpool wameidhinisha mkataba huo lakini haijulikani kama Suarez, mwenye umri wa miaka 26, atakubali kuendelea zaidi ya mwaka 2016, wakati mkataba wake utakapomalizika.

Meneja wa Liverpool Brendan Rodgers alisema hivi karibuni : " Suarez ni mwenye furaha hapa anacheza kwa tabasamu na shauku kubwa.

Mashabiki wanamuenzi na unaweza kuona uhusiano wao nae.."

Huenda ikahitajika mkataba wa karibu pauni £200,000 kwa wiki ikiwa maradufu ya pato lake la sasa kumshawishi kusaini kandarasi mpya. Hata hivyo uhusiano wake na maafisa wakuu wa Anfield umeimarika kwa kiwango kikubwa tangu alipojaribu kulazimisha auzwe Arsenal mwanzoni mwa msimu huu.

Arsenal ilijaribu mara mbili kumnunua Suarez bila mafanikio yoyote.

Lakini pia kumekua na fununu kwamba Real Madrid ya Uhispania nao pia wana hamu ya kumsajili.