MCHINA ATUMBUKIA SHIMONO NA KUFA

Raia mmoja wa Nchi ya China Chen Gungson mmiliki wa kampuni ya uchimbaji wa madini ya Got Accdent On Ming Camp amefariki dunia baada ya kutumbukia ndani ya shimo ambalo lilikuwa la mgodi wa dhahabu katika machimbo ya dhahabu ya Ibidi Wilayani Mlele Mkoa wa Katavi Tukio hilo la kutumbukia kwenye shimo la mgodi huo na kusababisha kifo cha Raia huyo wa China lilitokea hapo jana majira ya saa tatu na nusu asubuhi katika eneo hilo la Ibindi.

Raia huyo wa China alipatwa na mauti hayo wakati akiwa anakagua maeneo ambayo anafanyia shughuli zake za uchimbaji wa madini aina ya dhahabu na ndipo alipoteleza na kutumbukia ndani ya shimo hilo la mgodi wa dhahabu Baada ya kutumbukia jitihada za kumwokoa zilianza kufanywa na watumishi wenzake wakiwemo na raia wengine saba wa Raia wa China na wananchi wanaofanyashughuli kwenye maeneo hayo ambapo waliigiza kamba ndani ya shimo ili marehemu aweze kuishika na wao waweze kumvuta kwa nje Hata hivyo baada ya kuona kamba waliojaribu kumwokolea haija shikwa Raia wanne wa China waliingia ndani ya shimo hilo kwa kutumia kamba na waliweza kutoka na marehemu huyo na wao hawakujua kama ameishafariki dunia na kumbiza hospitali ya Wilaya kwa kutumia gari yao Aina ya TOYOTA Walipofika Hospitalini walimshusha haraka haraka marehemu kwa kutumia machela na kwenda kumlaza katika kitanda kilichopo wodi namba moja na kuwataka wauguzi wampe huduma ndugu yao huyo ya matibabu Mganga wa zamu Dokta Benald Mbushi alifika kwenye wodi hiyona alipompima Raia huyo wa China aliwaeleza kuwa Mchina huyo ameisha fariki hata kabla ya kufikishwa hospitalini hapo.

Kwa upande wake Dokta Benald Mbushi ameeleza kuwa mwili wamarehemu huyo umehifadhiwa katika chumba cha kuifadhi maiticha hospitali ya wilaya ya Mpanda ukisubili kufanyiwa uchunguzi kabla ya kukabidhiwa kwa ndugu zake.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi amethibitisha kutokea kwa kifo cha Raia huyo wa kutoka nchi ya China na ametowa wito kwa watu kutotembea karibu na mashimo ya migodi hasa katika kipindi hiki cha masika.