PADRI ANG'ANG'ANIWA KORTINI

KESI inayomkabili Padri Deogratius Makuri wa Kanisa Katoliki Jimbo la Singida kushindwa kutoa matunzo kwa mwanawe, kesi iliahirishwa tena kwa mara ya tatu baada ya mlalamikiwa kushindwa kufika mahakamani.

Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Utemini mjini Singida anayesikilizakesi hiyo, Ferdinand Njau alisema Padri Makuri ametuma mtu aliyedai kuwa ni dada yake kuja kuiarifu Mahakama kuwa hataweza kutokea kutokana na kuumwa.

Hata hivyo, Hakimu Njau alimwambia dada huyo na wasikilizaji kwa ujumla kuwa ili haki itendeke ni lazima mlalamikiwa awepo mahakamani. "Kuna baadhi ya watu wanasema kwa nini labda kesi hii isingesikilizwa faragha eti kisa tunasali naye."Hoja kwamba tunasali naye haipo hapa. Ndio maana nimeamua kesi hii isikilizwe Mahakama ya wazi. Nitasimamia kwa nguvu zangu zotenikizingatia sheria hadi haki ipatikane maana nipo kwenye mtego.…. huyu ni kiongozi wangu kanisani, sawa.

Lakini pia huyu mtoto, malaika wa Mungu, anahitaji matunzo.

Nisipotenda haki, Mungu atanihukumu," Hakimu Njau alisema.

Kutokana na umuhimu huo, Hakimu Njau alisema kuwa endapo mlalamikiwa hatafika tena Januari 3, 2014, ambapo kesi hiyo imepangwa kusikilizwa, atalazimikakusikiliza kesi hiyo upande mmoja.

Padri Makuri, ambaye pia alikuwa Katibu wa Askofu wakati huo, anatuhumiwa kushindwa kutunza mtoto wake mwenye umri wa mwaka mmoja na miezi minane aliyezaa na Maria Boniphace (26), mkazi wa eneo la Mitunduruni mjini hapa.