BUNGE LAAHIRISHWA, WAZIRI DAVID MATHAYO ATAKWA KUJIUZULU.

Kamati ya Lembeni ambaye amesoma Taarifa Uchunguzi ya Kamati kwa Bunge Hivi Punde imependekeza Waziri wa Maendeleo na Uvuvi, Dk David Mathayo David , Mkurugezi wa Wanyamapori na maofisa wengine wajiuzulu mara moja kutokana na kuwapo kwa matukio ya kuchomwa moto kwa nyumba za wananchi na kuuawawa kwa baadhi ya watu wakati wa operesheni tokomeza majangili.

Bunge Limeahirishwa kwa muda ili kujadili muda uliopendekezwa na Wabunge wa kujadili ripoti ya uchunguzi ya Lembeni kuhusu mauaji na nyumba kuchomwa moto wakati operesheni tokomeza majangili nchini.

Katika taarifa hiyo imependekeza Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Dk David Mathayo David ajiuzulu, mkurugenzi wa Wanyamapori Tanzania, maofisawa jeshi na mgambo kwa kuhusika katika mauaji hayo.

Wabunge wamehoji wakiwamo Zitto Kabwe (Chadema) kwanini kamati ya Lembeni inamtaka Dk David Mathayo David ajiulu wakati kuna viongozi wengi wanahusika katika kashfa hiyo.

Katika ripoti ya Lembeni imemruka Waziri wa Maliasili na Utalii, Hamisi Kagasheki na naibu waziri wake, pamoja na mawaziri wengine hawatajwa.

Kwa uamuzi wa Naibu Spika kuahirisha Bunge inamaanisha amekubaliana na hoja ya Tundu Lissu (Chadema) ya kuahirishwa Bunge hilo. Pia Mbunge, Ligora(CCM) naye alichangia hoja hiyo na wabunge wengine.