MAPIGANO BADO YAKIENDELEA SUDAN KUSINI

Wakati juhudi zikizidi kuendelea za kujaribu kumaliza mapigano Sudan Kusini, Msemaji wa Jeshi la Sudan Kusini amesema kuna matumaini madogo ya kusitishwa kwa mapigano.

Kiongozi wa waasi Riek Machar amesema wapiganaji wake bado wanashikilia eneo kubwa la Kaskazini mwa nchi, huku majeshi ya serikali yakisema yameukomboa mji wa Malakal na wamezingira eneo la Bentiu , mjimkuu wa jimbo la Unity.

Rais Salva Kiir amesema yupo tayari kusitisha mapigano mara moja, lakini hasimu wake Bwana Machar amesema mazungumzo zaidi yanahitajika kukubaliana kusitisha mapigano na kwamba yupo tayari kufanya mazungumzo iwapo serikali itakuwa tayari kuwaachia huru wanasiasa 11 wanaomuunga mkono ambao walikamatawa wakati vurugu zilipotokea.

Machar aliyasema hayo baada ya serikali kusema ipo tayari kusitisha mapigano makubaliano yaliyopokewa kwa mikono miwili na viongozi wa Afrika Mashariki mjini Nairobi.

Mapigano yaliendelea siku ya ijumaa katika mji wa Makalal, katika jimbo la Upper Nile.

Tayari askari zaidi wa Umoja wa Mataifa wa kuongeza nguvu wamekwisha wasili nchini Sudan Kusini.